Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nitalinda Hawa Wadosi: Ruto asema atawapa Uhuru na Raila usalama wakiondoka

04fec69efb13dbb6 Nitalinda Hawa Wadosi: Ruto asema atawapa Uhuru na Raila usalama wakiondoka

Sat, 25 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Licha kile kimetajwa kama tofauti kali baina ya Rais Uhuru na naibu wake, Ruto alisema atamlinda akiondokaAkizungumza huko Migori DP alisema Raila na Uhuru wamempangia njama kali ya kisiasa lakini ana imani atawawezaAlianzisha siasa za system na Deep State akisema Wakenya ndio wataamua kuhusu mshindi wa uchaguzi ujaoNaibu Rais William Ruto Jumamosi September 25 alisema atawaheshimu Rais Uhuru Kenyatta na kinara wa ODM Raila Odinga iwapo ataibuka mshindi wa urais 2022.

Ruto alisema atahakiksiha kuwa Uhuru na Raila wana maisha mazuri watakapokuwa kwani serikali yake itawalinda.

"Hawa wadosi mimi nitawachunga, nitawapatia askari ili walindwe, mnisaidie alafu mimi nitahakikisha wako sawa. Nitahakikisha wako na askari mingi mingi ili waweze kutembeatembea," alisema DP Ruto.

Alisema Raila na Uhuru anampangia kisiasa kwa kuwaleta pamoja Kalonzo Musyoka, Musalia Mudavadi, Gideon Moi na Moses Wetangula.

"Hawa jamaa wamenipangia, wamenipangia sana . . . wameunda kundi la watu saba. Lakini ni sawa tu, mimi niko na gang ya mamilioni ya hustlers. Mniombee sana hawa wadosi wawache kunilima," alisema Ruto.



Aidh DP Ruto alirejelea siasa za 'system na Deep State' akisema Wakenya ndio wataamua ni nani atakuwa rais.

"Mimi niko na mamilio ya hustlers, si nyinyi ndio mtaamua. Ni nyinyi sio deep state ama system," alisema Ruto.

"Hii si haki, eti mimi nimewasaidie alafu sasa imefika ni mimi hawataki, apana hiyo haiwezekani. Nimeamua wakati huu lazima niinue kina mama wa mboga na hsutlers," aliongeza DP.



Alisema alifika Migori kuwainua hustlers wenzake na akatoa msaada wa KSh 1.5M kusaidia vikundi vya wanabodaboda.

"Nimeambiwa hapa kuna makundi ya vijana wa bodaboda 48, mimi ninataka kuwasaidia ili waweze kujiinua. Sasa nimekuja na ninawapa KSh 1.5M ili waweke kwa sacco kujikuza," Ruto alisema huku akishangiliwa.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke