Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nitakuwa fala sasa kumuunga Raila mkono Kuwania Urais 2022, Kalonzo Asema

7063ce597713b0cd Nitakuwa fala sasa kumuunga Raila mkono Kuwania Urais 2022, Kalonzo Asema

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Musyoka amekanusha madai kuwa kuna mazungumzo yanayoendelea kati yake na Raila kuhusu kuwania urais 2022Kalonzo amekuwa mgombea mwenza wa Raila katika chaguzi za 2013 na 2017 chini ya muungano wa NASA lakini hawakufaulu kuingia IkuluAlisema ataonekana mjinga kumuunga mkono Raila kwa safari ya tatu mfululizo ilhali yeye hajarudisha mkonoWakati wa mazishi ya Kalembe Ndile Raila alisema wataongea na Kalonzo na yuko na imanai kuwa watapata mwafaka wa kufanya kazi pamojaKinara wa Wiper Kalonzo Musyoka amemtaka Raila Odinga na chama chake cha ODM kumuunga mkono kuwania urais 2022.

Kalonzo alisema 2022 unafaa kuwa wakati wa Raila kurudisha mkono kwani amekuwa akimuunga kuwania urais kama ilivyofanyika 2013 na 2017.

Kalonzo alisema hawezi kukubali kumpa Raila usaidizi ifikapo 2022 na ndoa yake na Raila itawezekana akikubali kumuunga mkono.

"Mimi si mwanasiasa dhaifu, na nitakuwa mmoja wa wajinga ulimwenguni iwapo nitakubali kumuunga mkono Raila kwa safari ya tatu bila yeye kurudisha mkono," alisema Kalonzo.



Kiongozi huyo alifichua pia kuwa hakujakuwa na mazungumzo yoyote kati yake na Raila Kuhusu 2022.

Wakati wa mazishi ya Kalembe Ndile, Raila alisema watazungumza na Kalonzo kuhusu 2022 akisema hawawezi kukosana.

"Mimi na Kalonzo tutaongea tu. Hatuwezi kukosana. Tutakubaliana tu, tutaelewana . . . " alisema Raila.

Matamshi ya Raila yalizua wasiwasi ndani ya muungano wa ONE Kenya Alliance unaomhusisha Kalonzo, Musalia Mudavadi, Gideon Moi na Moses Wetangula.

Wanne hao wamekuwa wakipanga karata yao wakisema wako tayari kuunga mmoja wao mkono ili kuingia Ikulu 2022.

Raila aliwafanya kuanza kushuku kuwa kuna kadi ambayo Kalonzo ameficha chini ya meza na huenda ataichomoa masaa ya lala salama.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke