Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nina watoto watatu lakini sipendi kuwaanika mitandaoni, Jalang'o

988c7fc431117643 Nina watoto watatu lakini sipendi kuwaanika mitandaoni, Jalang'o

Wed, 28 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mcheshi Jalang'o aliambia Ayo TV kwamba ana binti wawili lakini hapendi kuwaanika mitandaoniHata hivyo, katika tafuta tafuta kwenye mitandao utakutana na picha za mtangazaji huyo akiwa na binti zake wawiliVile vile kunazo baadhi ya blogu ambazo zimezungumzia maisha ya mcheshi huyo na familia yakeMengi yanajulikana kumhusu mcheshi maarufu na na mtangazaji wa redio Felix Odiwuor anayejulikana kwa jina la matani kama Jalang'o.

Mcheshi huyo ameangaziwa kwa kina tangu alivyolelewa katika familia maskini hadi alipoinuka kimaisha na vile vile kufunga ndoa ya kifahari.

Hata hivyo ni machache yanayojulikana kumhusu maisha yake ya kuwa mzazi wa watoto watatu.

Akizungumza akiwa AYO TV, Jalang'o alisema ana watoto watatu, mmoja na mpenzi wake waliyetengana na wawili katika ndoa yake ya sasa.

Alisema kwamba hapendi kuweka masuala ya familia yake kule nje kwa sababu anaogopa kuhukumiwa kimakosa na watu.

"Mimi ni kipenzi cha watu wengi lakini kuna baadhi pia wananichukia kwa hivyo sipendi kuanika familia yangu hadharani kwa sababu huenda wakashambuliwa," Jalang'o alidokeza.



Read also

Ubinafsi wa baadhi ya wanasiasa unahatarisha kwenye mapambano dhidi ya COVID-19

Alisisitiza kwamba kwa kuwa mtandao sio salama yuko radhi kuwaficha wanawe ndiposa kila wanapoenda wawe sawa na wenzao.

Kulingana naye, watoto wake watakapokuwa wakubwa watajiamulia maisha ambayo wanataka kuishi.

Jalang'o alijaliwa kifungua mimba wake Salika, ambaye ni binti na mwanahabari Cheptoek Boyo kabla ya uhisiano wao kukatika.

Ana watoto wengine wawili na mkewe Amina.

Katika mahojiano kwenye Runinga ya Ebru miaka minne iliyopita, Jalang'o alifichua kuwa hamu yake kubwa ni kufanya kazi kwa bidii ili watoto wake wasiwe na maisha magumu kama aliyopitia.

"Nataka siku moja wakiwa wakubwa watanionea fahari kwa bidii yangu kuwapa malezi mazuri," alielezea.

Mcheshi huyo alisema bidii yake inatokana na ugumu waliopitia wazazi wake kumpa elimu ambapo digrii yake ya kwanza aliipata akiwa mtu mzima.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.



Read also

Mafuriko yaliyotokea Ulaya, China yanatukumbusha umuhimu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke