Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nimempoteza mshauri wangu, Rais Kenyatta asema kumhusu Kaunda

A1938e8bfd928af4 Samatta asaini miaka mitatu Fenerbahçe

Sat, 3 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais alisema Kaunda alikuwa rafiki mkubwa wa babake Mzee Jomo Kenyatta na mshauri wake baada ya kifo cha MzeeKaunda alikuwa na miaka 97 na atazikwa katika kaburi la marais nchini humo ambapo wenzake watatu wamezikwaKiongozi huyo atasalia maarufu baada ya vazi lake kukubali kiwango cha kupewa jina lake na kujulikana na wengi kama 'Kaunda Suit'Rais Uhuru Kenyatta amemuomboleza aliyekuwa Rais wa Zambia Kenneth Kaunda kama mmoja wa watoto tajika wa Afrika.

Rais aliwasili mjini Lusaka Ijumaa Julai 2 ambapo aliungana na marais wengine katika sherehe ya kumpa mkono wa buriani.

Aliwasilisha rambirambi za Wakenya na Afrika kwa familia na raia wa nchi hiyo akisema Kaunda atakumbukwa kila kona.

"Leo nasema nimempoteza rafiki na sio rafiki tu ila mshauri wangu. Kenya tutamkumbuka kama rafiki mkubwa wa rais wa kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta," alisema Rais Uhuru.



Kaunda ndiye rais wa kwanza wa taifa hilo la Zambia na alifariki Juni 17 akiwa na miaka 97 na sasa atawafuata marais waliomtangulia.

Serikali nchini humu imesema kiongozi huyo atazikwa Julai 7katika kaburi la Embassy Park Presidential Burial site Lusaka ambapo marais waliofariki dunia mbele yake walizikwa.

Marais hao ni Levy Patrick Mwanawasa ambaye alikuwa rais wa tatu, Dr Fredrick Chiluba wa pili na Michael Sata wa nne.

Kiongozi huyo atakumbukwa na wengi haswa kutokana na vazi la suti lake ambalo lilipata umaarufu Afrika.

Nguo hiyo ilipewa jina lake na sasa hujulikana kama 'kaunda suit' kila eneo.

Alikuwa ni miongoni mwa marais wa kwanza kuchukua mamlaka katika Afrika kuwa hai.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke