Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nigeria yatangaza hali ya hatari ya uhaba wa chakula

Nigeria Yatangaza Hali Ya Hatari Ya Uhaba Wa Chakula.png Nigeria yatangaza hali ya hatari ya uhaba wa chakula

Fri, 14 Jul 2023 Chanzo: Bbc

Rais wa Nigeria Bola Tinubu ametangaza hali ya hatari kuhusu usalama wa chakula ili kukabiliana na mfumuko wa bei ya chakula unaoendelea.

Mikakati ya haraka, ya kati na muda mrefu imeundwa na serikali kukabiliana na uhaba huo.

Ikiwa ni pamoja na kutoa mbolea na nafaka kwa wakulima na kaya hadi kutoa jukumu la kutoa chakula na maji kwa Baraza la Usalama la Taifa.

Serikali inapanga kutenga fedha kutokana na kuondolewa kwa ruzuku ya mafuta kusaidia sekta ya kilimo na kuanzisha Bodi ya Kitaifa ya Bidhaa ili kudhibiti na kuleta utulivu wa bei za vyakula.

Rais Tinubu alisisitiza malengo ya mipango ya kupunguza gharama za chakula, kukuza kilimo na kuzalisha fursa za ajira.

Katika chapisho kwenye ukurasa wake wa Twitter, Rais Tinubu alisema kwamba "mipango mipya itakabiliana na kupanda kwa gharama za chakula, kuimarisha kilimo, na kuongeza ajira".

"Hakuna atakayeachwa nyuma katika juhudi zetu za kuhakikisha chakula cha bei nafuu na kingi kwa kila Mnigeria," alitweet.

Mapema mwezi huo, gavana wa zamani wa kaskazini mwa Nigeria alielezea wasiwasi wake kwamba nchi hiyo inaweza kukabiliwa na shida ya chakula hivi karibuni kutokana na ujambazi Kaskazini.

Shirika la Fedha Duniani lilionya juu ya kuongezeka kwa bei ya vyakula na hatari kutokana na mafuriko na mbolea ghali.

Chanzo: Bbc