Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Niger yazindua chanjo ya uti wa mgongo

Cameroon Yatoa Chanjo Ya Kwanza Ya Malaria Duniani Niger yazindua chanjo ya uti wa mgongo

Fri, 3 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Nchini Niger, kampeni ya chanjo ilizinduliwa Alhamisi huko Niamey ili kupambana na janga la homa ya uti wa mgongo. Tangu katikati ya mwezi Machi, zaidi ya wagonjwa 2,000, pamoja na vifo 123, zimerekodiwa nchini, katika mikoa ya Niamey, Agadez, Zinder na Dosso. Niger, iliyoko katika ukanda wa meninjitisi ya Kiafrika, hukumbwa na magonjwa ya mlipuko kila mwaka, lakini ukubwa wao hutofautiana.

Shirika la Afya Duniani linakadiria kuwa idadi ya kesi za homa ya uti wa mgongo kwa sasa inaongezeka kwa kasi nchini Niger ikiwa na ongezeko la 50% ikilinganishwa na mwaka jana na kiwango cha vifo cha 6%.

WHO inakumbusha kwamba ugonjwa wa meningitis, kuvimba kwa tishu zinazozunguka ubongo na uti wa mgongo, ni dharura ya matibabu. Dalili zake kuu ni homa, ugumu wa shingo, unyeti wa mwanga, maumivu ya kichwa na kutapika.

Ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu, ambao unaweza kusababisha kifo au kusababisha athari, mipango tayari inaendelea kama vile ufuatiliaji, utunzaji wa wagonjwa na hata chanjo.

Kampeni ilizinduliwa siku ya Alhamisi katika eneo la Niamey, kitovu cha janga hilo, na wastani wa wagonjwa 52 kwa kila wakaazi 100,000. Lengo la WHO na washirika wake ni kutoa chanjo kwa watu 900,000 wenye umri wa mwaka 1 hadi miaka 19. Mwaka huu, chanjo mpya inatumiwa, inasimamiwa kwa dozi moja. Ni nzuri dhidi ya aina 5 kuu z virusi vinavyosababisha homa ya uti wa mgongo nchini Niger.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live