Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

'Ni wanafunzi wa Nigeria pekee waliosalia hapa'

Hali Ya Utulivu Yarejea Sudan Makundi Hasimu Yakisitisha Mapigano 'Ni wanafunzi wa Nigeria pekee waliosalia hapa'

Wed, 26 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Raia wa Nigeria wanaonekana kuwa wanafunzi pekee wa kigeni waliobakia wamekwama nchini Sudan, mmoja ameambia BBC katika simu yake ya huzuni.

"Ni wanafunzi wa Nigeria pekee waliosalia hapa Sudan, kila mtu ameondoka, sisi tu," mwanafunzi wa chuo kikuu, ambaye hataki kutajwa jina, alisema.

Mataifa mengine ya Afrika kama Afrika Kusini, Kenya, Mali, Ivory Coast na Uganda ni miongoni mwa mataifa ambayo yametangaza kuwahamisha baadhi ya raia wao.

"Inasikitisha sana," aliendelea, akiongeza kwa sauti kwamba alitarajia Nigeria ingekuja kwa ajili yake na uokoaji wa wanafunzi wenzake hivi karibuni.

Alisema Nigeria iliendelea "kuchelewesha" kutumwa kwa mabasi ili kuwahamisha.

Alitarajia waje Jumanne, lakini hawakuwahi kufika. Kisha aliambiwa na ubalozi kwamba mabasi yangewachukua saa 06:00 kwa saa za huko leo, lakini walikuwa hawajawachukua hadi saa 10:00.

Aidha, Ubalozi huo ulisema ni mabasi matano pekee ndiyo yatawasili, lakini hiyo haitoshi kuwasafirisha wanafunzi wote, alisema.

Watu katika hosteli yake ya chuo kikuu pia walikuwa na upungufu wa chakula, alisema, na walikuwa wakijaribu tu kuishi: "Tuna njaa hapa."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live