Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ndoa ya mwimbaji wa injili yavunjwa baada ya miaka 21 bila ngono

42050f9eb3cc2ced Ndoa ya mwimbaji wa injili yavunjwa baada ya miaka 21 bila ngono

Tue, 6 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ndoa kati ya mwimbaji Rebecca Magaba, na Zabron Maselege ilivunjwa baada ya wanandao hao kudaiwa kuishi kwa miaka 21 bila kushiriki ngono

- Maselege anakumbana na tatizo la kutokuwa na nguvu ya kiume"cryptorchidism" hali ambayo mwanamume hana korodani zote mbili

- Mahakama hiyo ilisema ilivunja ndoa ya Rebecca na Maselege, baada ya kuona wanandoa hao wanafanya matendo ya ndoa ambayo si ya kawaida

Katika Kisa ambacho kimeduwaza wengi, mahakama moja nchini Tanzania imevunja ndoa ya miaka 21 bila kushiriki ngono.

Ndoa kati ya mwimbaji Rebecca Magaba, na Zabron Maselege ilivunjwa baada ya wanandao hao kudaiwa kuishi kwa miaka 21 bila kushiriki tendo la ndoa.

Kwa mujibu wa taarifa nchini humo, Maselege anakumbana na tatizo la kutokuwa na nguvu ya kiume"cryptorchidism" hali ambayo mwanamume hana korodani zote mbili na wala kutoa mbegu za kiume.

Mwanamume mwenye hali hii hana uwezo wa kupachika mimba.

Huku akitoa ushahidi kortini ya kutaka ndoa hiyo ivunjwe, Rebecca alisema walishindwa kushiriki tendo la ndoa katika kipindi cha miaka 21 kutokana na hali ya kiafya ya mume wake.

Rebecca, aliyetamba na wimbo wake wa Ebenezer, alisema walifunga ndoa ya Kikristo mkoani Mwanza mwaka 2002, lakini kabla ya ndoa hiyo hawakuwahi tofautiana wakati wa uchumba wao.

Baada ya kufanya harusi, walirudi nyumbani huku akiwa na hamu ya kujamiana na mumewe lakini mambo yalikuwa tofauti na matarajio yake.

Alitegemea kuwa wangefanya tendo la ndoa usiku huo lakini mume wake alilala na akidai kuwa amechoka kutokana na sherehe.

Lakini mambo yaliendelea vivyo hivyo kwa siku tano na ndipo alilazimika kwenda kanisani kumweleza mchungaji aliyewafungisha ndoa hiyo na mume wake alipohojiwa alisema alishikilia kuwa ni uchovu tu.

Baadaye wakiwa nyumbani kwao, mume wake aliamua kufunguka, alipanda kitandani na kumuonyesha sehemu zake za siri akifichua kuwa hana korodani zote mbili na hajawahi kutoa mbegu za kiume.

Rebecca alisema alimvumilia mume wake na waliishi kwa zaidi ya miaka 18 ya ndoa yao huku mume wake akifanyiwa matibabu.

Msanii huyo pia alieleza kwamba mumu wake alianza kumpiga na hivyo kuwapelekea kutengana.

“Mume wangu alivyoona kila mtu ameijua tabia yake, ndipo mwaka 2015 aliniambia tuhamie Dar es Salaam kutoka Mwanza. Tuliishi eneo la Segerea, lakini tabia yake ya kupiga iliendelea ndipo mwaka 2017 nilitengana naye rasmi,” alisema Rebecca.

Akitoa hukumu yake, Hakimu Mwinyiheri alisema Mahakama hiyo imevunja ndoa ya Rebecca na Maselege, baada ya kuona wanandoa hao wanafanya matendo ya ndoa ambayo si ya kawaida.

Mahakam pia iliamuru mali yote ambayo wanandoa hao walichuma pamoja igawanywe kwa usawa.

Shamba la eka 10 lililopo Bagamoyo (Pwani), maduka mawili yaliyopo Bonyokwa (Dar es Salaam), majengo na shamba la miti ya mikalatusi eka moja lililopo mkoani Kigoma zilipewa Maselege naye Rebecca akisalia na uwanja Dar es Salaam.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke