Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ndio Magufuli ametuacha ghafla lakini hayati alitufunza nini?

MAGUFULI 18?fit=1280%2C720&ssl=1 Ndio Magufuli ametuacha ghafla lakini hayati alitufunza nini?

Mon, 19 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kauli ya Mhariri: Makala haya ni kutoka kwa Amin Kweyu Watako ambaye ni mwalimu wa Kiswahili na mdadavuaji wa masuala ya lugha. Kumbuka kauli iliyotolewa hapa ni ya mwandishi binafsi wa makala haya na wala sio msimamo wa TUKO.co.ke.

Wanasema wanadini kuwa kuugua ni sunna lakini kuaga dunia ni faradhi. Vivyo hivyo, wanasema Waswahili kuwa chema hakidumu; na ukianguka mti mkuu basi ndege wake huwa mashakani! Ndio maana tumefunzwa katika dini zetu kuwa hapa duniani sote tu wapita-njia. Kwa maana hiyo ni kuwa sote tu mauiti. Twatembea tukiwa marehemu. Mola atujaalie tuwe na mwisho mwema sisi waja wake.

Pia Soma: Mwaka Mmoja Tokea Kifo cha Walibora, Twamkumbuka Vipi Marehemu!

Siku si nyingi zilizopita, tulikuwa naye rais wa Tanzania, mtu mchapa-kazi, mwenye nguvu, siha na bidii ya mchwa. Akitumbua majipu hadi kubatizwa jina la buldoza. Lakini yu wepi Magu? Wanaomboleza Watanzania! Linatokwa na chozi bara la Afrika! Dunia inalia kwi!

Pili, niseme kuwa ni miiko sisi Waafrika, na mafunzo yalivyo ya dini zetu kuwa akifariki dunia mtu tunamwombea safari njema huko akhera. Nasi pia kujiombea mwisho mwema. Ndivyo tunavyomfanyia ndugu yetu Magu. Kifo chake kimeifanya Tanzania kuwa na rais wa kwanza mwanamke, mama Samia Suluhu Hassan, mzaliwa wa visiwa vya Zanzibar. Makao makuu ya karafuu. Napata kumbukizi zangu nikiwa visiwani Zenji, ni miaka mingi sasa.

Pia Soma: Hizi Bei za Mafuta Zinatukandamiza, Wakenya Tunaumia Sana Serikali!



Kila la kheri mama Samia. Akuongoze Mola.

Tatu, nchi ya Tanzania inapokuwa ikiomboleza, ni vizuri kukumbushana kuwa majonzi hayo yametufika pia na sisi. Hasa nikizikumbuka kauli zake hayati Magufuli, utaya unalowa chozi! Naikumbuka kauli hii hadi sasa. Alisema hayati Magufuli kuwa nchi ya Kenya ni nchi nzuri. Hata hivyo, inaweza kuwa nchi bora zaidi duniani mradi tu tupate suluhu ya donda-ndugu la ukabila! Mkenya mwenzangu upo? Tulia hapo ulipo. Utuame na kutafakari. Kauli hii ya hayati Magufuli inatiliwa pondo na kauli kama hiyo ambayo pia ilitolewa na rais wa kwanza wa Tanzania, hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Nchi ya Kenya ni kisawe cha ukabila. Hilo halina mjadala, mdahalo wala ubishi. Unabisha!?

Nne, hayati Magufuli amelithibitishia bara la Afrika kuwa janga la ufisadi linaweza kukabiliwa hadi likasalimu amri. Angalia alivyoitunza migodi ya nchi yake. Tazama alivyowadhibiti viongozi wafisadi. Akazuia safari za danganya-toto za nje ya nchi. Akayaokoa mamilioni ya pesa yaliyokuwa yakiliwa kwenye mirija ya ufisafi kwenye sherehe za kitaifa.

Pia Soma: Jameni serikali fungueni pingu za mashabiki wanataka kuingia viwanjani

Tano, hayati Magufuli ameudhihirishia ulimwengu kuwa nchi ya Tanzania, na nchi nyinginezo za Afrika, zinaweza kujimudu kiuchumi pasina kulitegemea pakubwa bakuli la omba omba. Hii inamaanisha kuwa madini, rasilmali na utajiri wa bara la Afrika ni mwingi mno hivi kwamba hatuhitaji kuomba misaada. Lakini viongozi wa nchi za bara la Afrika ni nani?

HITIMISHO: Hayati ni mtu ambaye kwamba amefariki dunia ambapo anakumbukwa kwa matukio yake wakati wa uhai wake. Anaweza kuwa rais, kiongozi, mfamle, shujaa n.k.

Makala haya yameandikwa na Amin Kweyu, unaweza kuwasiliana naye kupitia [email protected].

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke