Ndege ya kijeshi aina ya chopa imeanguka eneo la Oltinga kaunti ya Kajiado na kulipuka motohata hivyo, haijabainika ni abiria wangapi walikuwemo.
Kamanda wa polisi kaunti ya Kajiado Muthuri Mwongera amesema ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa mbili asubuhi siku ya Alhamisi, Juni 24
Muthuri alisema ndege hiyo ililipuka moto baada ya kuangaka kilomita 60 kusini mwa eneo la Oloopolos.
" Nimemtuma OCPD wa Kajiado Magharibu Vincent Kitili kwenda eneo la tukio kule Oltinga ili atuletee habari zaidi kuhusu yaliyojiri," Muthuri alisema.
Muthuri pia alithibitisha kwamba ndege hiyo ilikuwa katika shughuli ya mafunzo na inahofiwa kuwa huenda abiria wote wameangamia.
Shughuli za uokoaji zinaendelea.
Mengi kukujuia...