Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ndege ya Uganda yaishiwa mafuta Dar es Salaam

22e788ece38b3470 Ndege ya Uganda yaishiwa mafuta Dar es Salaam

Wed, 14 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Abiria katika ndege ya Uganda Airlines walichelewa safarini Jumatatu, Julia 12 jioni katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Shirika la ndege hiyo lilieleza kwamba kisa hicho kilisababishwa na kucheleshwa kwa mafuta yaliyokuwa yakipelekwa katika uwanja huoAidha shirika hilo liliomba radhi na kuahidi kutoshuhudiwa kwa kisa kama hicho siku za usoniAbiria katika ndege ya Uganda Airlines walichelewa safarini katika uwanja wa kimtaifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam nchini Tanzania baada ya ndege hiyo kuishiwa mafuta.

Shirika hilo lilieleza kwamba kisa hicho kilichotokea Jumatatu, Julai 12 jioni kilisababishwa na kucheleshwa kwa mafuta yaliyokuwa yakipelekwa katika uwanja huo.

Aidha uongozi wa kampuni hiyo ya ndege uliandika taarifa katika mitandao ya kijamii kuomba radhi kwa tukio hilo huku ikitoa ahadi ya kutorudia tena.

"Tunaomba radhi kwa kuwachelewesha abiria wetu katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana Julai 12 katika ndege ya UR 321. Huduma zetu zilitazika kufatia kucheleshwa kwa mafuta yaliyokuwa yakipelekwa katika uwanja huo kutoka kwa muuzaji wetu huko Dar es Salaam," taarifa hiyo ilisema.



Read also

Mtahiniwa wa KCSE Ajitoa Uhai Baada ya Kuandikia KNEC Barua

Kwingineko rubani mmoja alipoteza maisha baada ya kuhusika kwenye ajali ya ndege katika msitu wa Eburu eneo la Jerusalem, Ndabibi mjini Naivasha.

Ndege hiyo ambayo ilikuwa imewabeba abiria watatu ilianguka siku ya Julai 12 na kuwaka moto, ilikuwa imetokea uwanja wa ndege wa Wilson ikielekea Lodwar.

Abiria wawili waliachwa na majeraha mabaya na walikimbizwa katika hospitali ya kata ndogo ya kaunti ya Naivasha.

Akithibitisha kisa hicho, Kamanda mkuu wa polisi Beatrice Kiragu alisema ajali hiyo ilisababishwa na hali mbovu ya hali ya anga.

Iliripotiwa kwamba ndege hiyo ilikuwa inaelekea sehemu hiyo kuchunguza uvamizi wa nzige.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.



Read also

Mke Mwema: DP Ruto Asema Mkewe Rachael ni Kama Malaika, Nguzo ya Jamii Yake

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke