Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nataka kura yake pekee, Raila asema kuhusu Rais Uhuru 2022

9cdb9946ff42ebb5 Nataka kura yake pekee, Raila asema kuhusu Rais Uhuru 2022

Thu, 8 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Baba alisema yeye hategemei kuungwa mkono na Rais Kenyatta kwenye mapambano ya kuingia Ikulu 2022Alisema anachohitaji kutoka kwa kiongozi wa taifa labda kura yake na kwingine atajitetea kama wengineWandani wa Raila wamekuwa wakisema huu ni wakati mwafaka wa kuchukua mamlaka kwa sababu ako na 'system'Kinara wa ODM Raila Odinga Alhamisi Julai 8 aliweka wazi azma yake ya kuingia Ikulu kumrithi Rais Uhuru Kenyatta.

Akiongea na redio Citizen, Raila alisema yeye hajawahi kusema kuwa ana 'risasi moja' na kwa hivyo atakuwa debeni ifikapo 2022.

"Mimi sikusema niko na risasi moja, sijasema niko na risasi moja, niko na magazine kubwa,” alisema kiongozi huyo wa ODM.

Raila pia aliweka wazi kuwa hategemei uungwaji mkono na Rais Uhuru Kenyatta kwenye kura ya kuingia Ikulu wakati huo.

Alisema anachohitaji kutoka kwa Rais labda kura yake binafasi kama vile atawaomba Wakenya wengine.

Sijasema nataka endorsement ya Uhuru, ile kitu nitahitaji labda ni kura yake,” aliambia mwanahari Vincent Ateya wakati wa mahojiano hayo.

Kumekuwa na ripoti kuwa kinara huyo yuko kwenye mkataba wa handisheki na Rais ili 2022 aweze kupata uungwaji mkono.



Kulikuwa na ripoti hapo awali kuwa Rais ameahidi kuunga mkono mgombea wa muungano wa NASA kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Ni ripoti ambazo zilimchoma roho Naibu Rais William Ruto na kumfanya kulalamika kuwa licha ya kusimama na Uhuru kuanzia 2013 ameamua kuunga mkono waliokuwa wapinzani wao.

Wandani wa Raila nao wamekuwa wakisema 2022 utakuwa wakati bora wa kuchukua serikali kwani sasa Raila ni rafiki wa Rais Uhuru na kwa hivyo 'system' iko na yeye.

Je! Unayo hadithi kubwa ambayo ungependa tuchapishe? Tafadhali tuwasiliane kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690. Wasiliana na Tuko.co.ke papo hapo
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke