Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nameless amshukuru Mungu kwa kuwaponya wazazi wake kutokana na COVID-19

Edcc762087c5aa39 Nameless amshukuru Mungu kwa kuwaponya wazazi wake kutokana na COVID-19

Tue, 27 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Nameless alimshukuru Mungu kwa kumwezesha babake kutimia umri wa miaka 85

- Mwanamuziki huyo pia alimshukuru Mungu kwa kuwaponya wazazi wake kutokana na virusi vya COVID-19

- Kulingana na Nameless, mamake alipona haraka kufuatia collabo mpya aliofanya na mkewe Wahu

Mwanamuziki David Mathenge almaarufu Nameless pamoja na familia yake wanasherehekea baada ya baba yao kutimia miaka 85.

Nameless aliwajuza mashabiki wake kuhusu siku ya kuzaliwa ya babake kupitia mitandao ya kijamii Aprili, 27.

Akiwa mwingi wa furaha, Nameless alipakia video mitandaoni akiwa na wakati mwema pamoja na wazazi wake.

Namelesss alisema Mungu amekuwa mkuu na mwaminifu katika familia yao kwani babake amefanyiwa upasuaji mara mbili na yote ilifanikishwa na madaktari.

"Leo ni siku muhimu sana kwa familia ya Mathenge, babangu ametimia miaka 85, tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu, kama mnavyofahamu, babangu amekuwa akiugua tangu mwaka jana baada ya kufanyiwa upasuaji mara mbili," Alisema Nameless.

Nameless pia alifichua kwamba wazazi wake walipatikana na virusi vya COVID-19 baada ya kupimwa majuma kadhaa yaliopita.

Hata hivyo, Nameless alisema mamake aliweza kupona haraka kwa ajili ya kutizama wimbo mpya alioutoa hivi majuzi akiwa ameshirikiana na pamoja mkewe, 'Te Amo'.

" Kuongezea, Babangu na mamangu walikutwa na virusi vya covid-19, ulikuwa wakati mgumu kwa familia kwa sababu wazazi wangu wote wanaugua maradhi menigine. Nashukuru Mungu wote walipona wiki iliyopita baada ya Mama kulazwa hospitalini kwa siku kadhaa,

"Babangu naye hakuonyesha dalili za kuwa na virusi hivyo, hapo lazima niseme Amina, tunamshukuru Mungu kwa afya yao. mkiona tukisakata densi tukiwa na tabasamu kubwa kwa nyuso zetu, jueni tu tuna mengi ya kushukuru na kufurahia.

"Mamangu alisema alifurahia sana kutuona mimi na mke wangu kushirikiana pamoja kutoa wimbo, kulingana na , hatua hiyo ilimfanya apona haraka , kwa hivyo ningependa kumtakia babangu heri njema siku yake ya kuzaliwa. Happy Birthday Day Daddy"." Aliongezea Nameless.

Nameless na mkewe Wahu hakuwa wamefanya collabo kwa zaidi ya miaka 15 ambayo wamekuwa katika sekta ya uimbaji.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke