Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

"Nakupenda Sana Beby; mwanamuziki Samidoh ampamba mkewe na mapenzi

790463f41116a1e0 "Nakupenda Sana Beby; mwanamuziki Samidoh ampamba mkewe na mapenzi

Mon, 12 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Nyota wa muziki wa Mugithi, Samidoh Muchoki amewafurahisha Wakenya baada ya kumpamba mke wake Edith Nderitu na mapenzi kwenye runinga

- Msanii huyo anayesifika kwa wimbo Mumbi alikuwa mgeni kwenye shoo ya Churchill siku ya Jumapili ambapo alizungumzia taaluma yake kama polisi, mwanamuziki na pia familia

- Samidoh na Edith watakuwa wanaadhimisha miaka 10 katika ndoa hivi karibuni

Nyota wa muziki wa Mugithi, Samidoh Muchoki amewafurahisha Wakenya baada ya kumpamba mke wake Edith Nderitu na mapenzi kwenye runinga.

Msanii huyo anayesifika kwa wimbo Mumbi alikuwa mgeni kwenye shoo ya Churchill siku ya Jumapili ambapo alizungumzia taaluma yake kama polisi, mwanamuziki na pia familia.

Samidoh, amekuwa akigonga vichwa vya habari baada ya video yake akiwa na hawara wake Karen Nyamu kusambaa, alisema hakuna chochote ambacho kitabadilisha ukweli kwamba mtoto aliyezaa nje ya ndoa ni wake.

Alikubali makosa yake na kusonga mbele na maisha.

Akiulizwa kitu ambacho hajawahi kumuambia mke wake alimumiminia sifa akisema:

"Wakati sakata hiyo ilitokea alinisaidia sana. Tayari nilikuwa nimemwambia na nilipomuomba msamaha, niliamua kutofuatilia nilihisi kwamba kuna watu ambao walikuwa dhidi ya taarifa yangu," alisema.

Akiongezea kuwa:

"Wewe ni nguzo muhimu sana katika maisha yangu.Kutokana na ukweli kwamba wewe ni muombezi imesaidia. Asante sana, nakupenda sana."

Samidoh na Edith watakuwa wanaadhimisha miaka 10 katika ndoa hivi karibuni.

Awali, Tuko.co.ke iliripotia namna Samidoh alimuomba mke wake msamaha huku akikubali makosa yake.

“Poleni! Nimeiweka familia yangu na mimi mwenyewe katika hali mbaya. Ni kweli nilikuwa na uhusiano na Bi Karen Nyamu, na ni kupitia urafiki huo mtoto asiye na hatia alizaliwa,"alikiri Samidoh.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke