Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nairobi yashuhudia mvua kubwa iliyonyesha usiku kucha

E7e5ab6ed6362379 Nairobi yashuhudia mvua kubwa iliyonyesha usiku kucha

Mon, 10 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Nyingi ya barabara za jiji zilifurika maji kufuatia mvua kubwa iliyonyesha usiku kucha

- Kutokana na mafuriko yaliyokuwapo, dereva hakuweza kujua uwepo wa mtaro huo na ndiposa gari lake likaingia kwenye mtaro na kusakama

- Ujenzi wa Barabara Kuu ya Nairobi almaarufu Nairobi Expressway umechochea mafuriko ambayo awali hayakuwapo kwa mvua za aina hii na hili ni kwa sababu ya kutatizwa kwa mfumo wa maji taka ambao bila yaka utarekebishwa kwenye kazi zinazoendelea

Watu katika maeneo mengi ya mitaa ya jiji la Nairobi waneelezea kupata hasara kufuatia mvua kubwa iliyonyesa usiku kucha kuamkia Jumatatu, Mei 10.

Miongoni mwao ni madereva waliokuwa nje kabla ya saa za kafyu kufika na wengi walipatwa na mvua barabarani huku dereva mmoja akinusurika kifo baada ya gari lake aina ya Toyota Prado kuingia kwenye mtaro kwenye Mzunguko wa Nyayo .

Nyingi ya barabara za jiji zilifurika maji na kwa mujibu wa picha ambazo TUKO.co.ke imefanikiwa kuziona, dereva huyo alipoteza mwelekeo katika Barabara ya Bunyala ambayo hapo awali ilikuwa imefungwa na Mamlaka ya Barabara Kuu Nchini (KeNHA), na gari lake nusura kusombwa na maji.

Kutokana na mafuriko yaliyokuwapo, dereva hakuweza kujua uwepo wa mtaro huo na ndiposa gari lake likaingia hapo na kukwama. Mtaro huo ulichimbwa kwenye Barabara Kuu ya Uhuru.

Tukio hilo limejiri wiki mbili tu baada ya KeNHA kuzungusha sehemu ya Barabara Kuu ya Uhuru kwa waendesha magari ili kuruhusu kukamilika kwa barabara kuu ya Nairobi ambayo inajengwa.

Mapema Aprili, mahali hapo palifungwa kwa siku 20 kabla ya siku zingine 21 za ziada kuongezwa Ijumaa, Aprili 30 ili kuruhusu kukamilika kwa kazi ya ujenzi.

Kwa sababu ya ujenzi na kufungwa kwa sehemu hiyo ya barabara, madereva walitakiwa kutumia barabara ya kutoka Uwanja wa Nyayo hadi barabara ya Lusaka, Barabara ya Workshop na kuingia Barabara ya Bunyala kabla ya kuendelea na Barabara Kuu ya Uhuru.

"Madereva wa magari wanashauriwa kutumia njia mbadala. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote ambao unaweza kusababishwa tunapojitahidi kutengeneza barabara nzuri, salama na za kuaminika," barua kutoka mamlaka hiyo ilisema.

Waendeshaji magari wanaotumia Barabara Kuu ya Uhuru na Barabara ya kuelekea Mombasa wamelazimika kupambana na misongamano kutokana na leni kadhaa kufungwa na kuachwa leni chache.

Hali imekuwa mbaya zaidi kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha ambayo imesababisha mafuriko kando ya barabara ya kuelekea Mombasa na kueka bayana mfumo mbaya wa mifereji ya maji taka jijini Nairobi katika.

Ujenzi wa Barabara Kuu ya Nairobi almaarufu Nairobi Expressway umechochea mafuriko ambayo awali hayakuwapo kwa mvua za aina hii na hili ni kwa sababu ya kutatizwa kwa mfumo wa maji taka ambao bila yaka utarekebishwa kwenye kazi zinazoendelea.

Sehemu zilizoathiriwa zaidi ni pamoja na eneo karibu na Bellevue/Makutano ya South B, Imara Daima/City Cabanas na Mzunguko wa Nyayo.

Familia 300 hadi sasa zimeachwa bila makao tangu mvua zilipoanza katikati ya mwezi Machi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke