Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Naibu Rais Ruto awaonya viongozi wanaozidi kuuungana kisiasa

877db81adbda077e DP Ruto awasuta viongozi wanaozidi kuunda miungano ya siasa

Wed, 18 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

DP alisema Wakenya wanataka viongozi walio na mipango na sera za kuboresha maisha yaoRuto alisisitiza kuhusu umuhimu wa kuunda vyama vilivyo na sura ya kitaifa na ambavyo ajenda yake kuu ni kuboresha maisha ya wananchiNaibu Rais William Ruto amepuuzilia mbali kuundwa kwa miungano ya kisiasa kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka ujao, akitaja miungano hiyo ishara ya kushindwa.

Akizungumza Jumanne alipokutana na viongozi wa dini kutoka Tharaka Nithi nyumbani kwake Karen Jumanne, Agosti 17, DP alisema Wakenya wanataka viongozi walio na mipango na sera za kuboresha maisha yao.

"Wanatumia mikakati ya kizamani kuepuka kushindwa. Enzi za kuunda vikundi vya siasa na kuidhinishwa umekwisha," Ruto alisema.

"Nitashindwaje kuwashinda ikiwa bado mnashirikiana katika vyama vya kikabila visivyo na ajenda ya kuipeleka Kenya mbele."

Ruto alisisitiza kuhusu umuhimu wa kuanzishwa kwa vyama vya kitaifa vilivyoundwa kwa kanuni thabiti za kijamii na kiuchumi ili kuleta utulivu wa siasa nchini.

Read also

Raila Apokelewa kwa Shangwe Kaunti ya Nakuru, Asema Safari ya 2022 Imeanza

Aliwataka viongozi kujiepusha na siasa za zamani za kikabila ambazo zitaharibu sura ya kijamii na ajenda ya maendeleo.

Viongozi waliokuwa katika mkutano huo Karen walimhakikishia DP kuwa wataunga mkono azimilio lake na pia kuhakikisha wakazi wa Tharaka Nithi wanasimama nyuma yake.

"Tutaendelea kujipanga ndani ya United Democratic Alliance ambacho ni chama cha kitaifa kilicho na mipango thabiti ya maendeleo," Mbunge wa Kaunti ya Tharaka Nithi, Beatrice Nkatha, alisema.

Viongozi wengine waliokuwepo katika mkutano huo ni pamoja na; Wabunge George Murugara (Tharaka), Patrick Munene (Chuka / Igembe Ng’ombe), Gathoni Wa Muchomba (Mwakilishi wa Mwanamke, Kiambu) na Kimani Ichung’wah (Kikuyu).

Jumatatu Agosti 16, Ruto alikutana na viongozi kutoka Kaunti ya Meru wakiongozwa na Seneta Mithika Linturi nyumbani kwake Karen.

Alikutana pia na viongozi kutoka Kaunti ya Kisii wakiongozwa na Naibu Gavana Joash Maangi na Jaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki Charles Nyachae.

Wengine waliokuwepo walikuwa; Mbunge wa Bomachoge Chache Alfah Miruka, Mbunge wa Mugirango Kusini Sylvanus Osoro, Mbunge wa Zamani wa Mugirango Kusini Omingo Magara na wakili Cliff Ombeta miongoni mwa wengineo.

Read also

Picha za Kuhuzunisha za Mazishi ya Kaka 2 Waliouawa Embu na Polisi

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke