Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

NASA ilikufa ni wakati wa kutafuta marafiki wapya, Mudavadi asema

6143d67d9708a71e NASA ilikufa ni wakati wa kutafuta marafiki wapya, Mudavadi asema

Mon, 19 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Akizungumza wakati wa ibada ya kanisa Jumapili, Julai 18, Mudavadi alisema: "NASA ni historia, ni ya zamani sasa na tuendelee mbele, tujenge ushirikiano mpya,"Naibu Rais William Ruto, akizungumza katika Kaunti ya Kwale, alisema juhudi za kubadilisha katiba kupitia BBI ni kinyume cha sheriaKiongozi wa ODM Raila Odinga aliwashutumu wanaopinga BBI kwa kusema ni wale wale waliopinga Katiba ya 2010Kiongozi wa chama cha Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi alihitimisha safari yake ya siku mbili eneo la Mlima Kenya kwa tamko kwamba NASA imekufa na anatafuta ushirikiano mpya.

Hii ilijiri siku moja baada ya kusema kuwa kulikuwapo na mazungumzo ya kufufua muungano huo wa kisiasa na kumaliza tofauti kati yao.

Tofauti hizo zikiwa ni pamoja na suala kuhusu mapato kutoka kwa mgao wa pesa za vyama vya siasa ambapo vyama washirika wa NASA vinashtumu Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) kwa kujilimbikiza pesa hizo.

Akizungumza wakati wa ibada ya kanisa Jumapili, Julai 18, Mudavadi alisema: "NASA ni historia, ni ya zamani sasa na tuendelee mbele, tujenge ushirikiano mpya,"



Read also

DP Ruto Atoa Kauli Yake Kuhusiana na Uchaguzi wa Kiambaa

Kwa upande wake Seneta wa Nairobi Johnson Sakaja, ambaye ni mwanachama wa Chama cha Jubilee alisisitiza kuhusu urafiki baina ya vyama na wanasiasa.

"Unaangalia zamani au siku zijazo… tunataka kujenga urafiki mpya, NASA ni ya zamani, njoo siku za usoni,"

Viongozi kutoka eneo la Kati walioandamana na Mudavadi walisema kuwa Mlima Kenya uko tayari kufanya kazi na mtu yeyote ambaye atakuwa na masilahi yao moyoni.

"Tutakutana huko Sagana, na hapo ndipo tutafanya uamuzi kama jamii. Kwa hivyo mtu yeyote asizunguke akisema tayari wamepata kura za Mlima Kenya,” mbunge wa Kieni Kanini Kega.

Huko Pwani, siasa kuhusu Mchakato wa Salamu ya Maridhiano (BBI) na suala la kubadilisha katiba vilizungumziwa kwa kina.

Naibu Rais William Ruto, akizungumza katika Kaunti ya Kwale, alisema juhudi za kubadilisha katiba kupitia BBI ni kinyume cha sheria.

“Shida ya Kenya sio katiba, shida ya Kenya ni uchumi. Ata tukibadilisha katiba wapatiane vyeo, wagawane mamlaka, mwananchi mdogo hatakuwa katikati ya mambo ya vyeo na mamlaka,” alisema.



Read also

Tumepata Funzo: Ngunjiri Wambugu Asema Baada ya Kukaangwa Kiambaa

“Lakini tukibadilisha katiba na ipatikane kazi na biashara, kila mwananchi atachangia ndio Kenya itabadilika na sote tutakwenda mbele.”

Katika kaunti hiyo hiyo, kiongozi wa ODM Raila Odinga aliwashutumu wanaopinga BBI kwa kusema ni wale wale waliopinga Katiba ya 2010.

“Wengine wanaongea eti BBI inazidisha tu vyeo…BBI inapunguza gharama ya serikali, haizidishi, maanake mawaziri wengi watakuwa ni wabunge. Mishahara yao itakuwa ni ile ya bunge, ata waziri mkuu atakuwa mbunge,” alisema waziri mkuu huyo wa zamani.

Raila, aliyekuwa akihudhuria hafla ya mazishi ya Mzee Chitembe Bundu, aliongeza kuwa, ushindi wa BBI utakuwa wa Wakenya kwa kuwa utawezesha pesa zaidi kuingia mashinani.

“BBI italeta pesa ya kusaidia vijana mashinani, ambapo vijana wanaweza kwenda kukopa pesa na hawalipi riba mpaka baada ya miaka saba. Alafu vijana ambao watapewa mkopo ya kulipa karo katika vyuo vikuu vilevile hawatadaiwa chochite mpaka baada ya miaka minne ikiwa wamepata kazi na ajira ya kupata pesa,” aliongeza.



Read also

Magazeti Ijumaa: Babu wa Miaka 93 Afunga Ndoa na Kipusa wa Miaka19

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke