Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mzee ajisalimisha kwa polisi baada ya kumuua mwanawe

B7c8f903296f6157 Mzee ajisalimisha kwa polisi baada ya kumuua mwanawe

Wed, 14 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mshukiwa alimkabili mtoto wake, Allan Njiru, 40, akimtuhumu kukata mti bila idhini yake

- Baada ya wawili hao kubishana kwa muda mzee alichukua rungu akampiga mwanawe kichwani hadi kufa

- Mshukiwa anazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kianyaga

Polisi huko Kirinyaga wanamzuilia mwanamume wa miaka 70 kwa madai ya kumuua mwanawe kufuatia mzozo wa nyumbani.

Mshukiwa anazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kirinyaga kulingana na Daily Nation.

Kulingana na mashuhuda, mshukiwa alimkabili mwanawe, Allan Njiru, 40, akimtuhumu kukata mti bila idhini yake.

Baada ya wawili hao kubishana kwa muda mzee alichukua rungu akampiga mwanawe hadi kufa.

Walioshuhudia kisa hicho walisema mshukiwa alimpiga mwathiriwa mara kadhaa kichwani na silaha hiyo nzito na kumfanya apoteze fahamu.

Baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alijisalimisha kwenye polisi ambapo alizuiliwa na kuhojiwa.

"Mhasiriwa alikata mti na akauuza. Hatua hiyo ilimkasirisha babake kwa sababu hakuomba ruhusa," mmoja wa mashuhuda, Jane Wamunyu, alisema.

Mkuu wa polisi wa Kirinyaga Mashariki Anthony Wanjuu alisema kmshukiwa atakabiliwa na shtaka la mauaji.

"Mshukiwa alifika kituo cha polisi na kukiri kwamba alimshambulia vibaya mtoto wake. Huenda akashtakiwa kwa kosa la mauaji," alisema.

Aliwaonya wazazi dhidi ya kushambulia wanao dhidi ya mizozo ambayo inaweza kutatuliwa.

"Wazazi wanapaswa kujizuia wanapokerwa na watoto wao ili kuepusha visa kama hivi," alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke