Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

TV

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mweneshaji wa kituo cha watoto atuhumiwa kuwanyanyasa kingono

Teresia Wambui Fdv Mweneshaji wa kituo cha watoto atuhumiwa kuwanyanyasa kingono

Thu, 3 Oct 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwendeshaji wa kituo cha kulelea watoto Kiambu afikishwa mahakamani kwa kutumia watoto kutengeneza video za ngono.

Mwanamke anayesimamia kituo cha kulelea watoto katika Soko la Wangige, Kaunti ya Kiambu, amekamatwa kwa tuhuma za kuwadhulumu kingono watoto wadogo.

Kulingana na nyaraka za mahakama, kituo hicho kinachoendeshwa na Teresia Wambui Kihagi kwa miaka mitatu kimekuwa na zaidi ya watoto 10, ambao wote wanaaminika kuwa waathirika wa vitendo hivyo vya kikatili.

Alipofikishwa mahakamani Jumanne, mahakama iliambiwa kwamba simu ya Kihagi ilichukuliwa wakati alipokuwa akijaribu kuharibu ushahidi kwa kuivunja, lakini sasa ushahidi huo utaopolewa na kuchakatwa ili kutumika mahakamani.

"Nyaraka za mahakama zinaeleza kuwa mtuhumiwa amekuwa akiwahusisha watoto wenye umri kati ya miaka miwili na minne katika vitendo vya ngono, akiwagusa sehemu za siri na kurekodi video za vitendo hivyo akiwa katika kituo hicho cha kulelea watoto," ilisema sehemu ya nyaraka za mahakama.

Afisa mpelelezi Nicodemus Musembi alisema uchunguzi utafanywa kwenye namba za simu za mtuhumiwa ili kubaini walengwa wa video hizo na pia kuangalia kwa undani matumizi ya Paybill ya Equity iliyotumiwa na kituo chake.

Musembi aliendelea kusema kuwa kuchukua taarifa kutoka kwa wazazi waathirika haikuwezekana na uchunguzi utafanywa kupitia kwa mpatanishi.

Kwa hivyo, aliomba mtuhumiwa azuiliwe kwa siku 21 ili kutoa nafasi ya uchunguzi zaidi, huku akiendelea kufanyiwa uchunguzi wa afya ya akili.

Wakati huo huo, waathirika wamepelekwa kwenye vituo mbalimbali vya afya kwa uchunguzi wa kimatibabu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live