Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanawe marehemu seneta Yusuf Haji ahitimishwa kugombea useneta Garissa

857e907eaf94a6c6 Mwanawe marehemu seneta Yusuf Haji ahitimishwa kugombea useneta Garissa

Thu, 1 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mwanawe aliyekuwa seneta wa Garissa Marehemu Yusuf Hadji amepokezwa cheti cha kuwania kiti cha useneta kaunti ya Garissa

- Abdikadir amewashukuru wananchi pamoja na viongozi wa kaunti ya Garissa na kuahidi kwamba atachapa kazi ipasavyo iwapo atachaguliwa kuwa seneta

- Kiti cha Useneta cha Garissa kiliwachwa wazi kufuatia kifo cha Yussuf Haji

Aliyekuwa mwanawe seneta wa Garissa Yusuf Haji, Abdikadir Mohammed Yusuf aliidhinishwa na tume ya uchaguzi ya IEBC kugombea kiti cha useneta wa kaunti hiyo.

Kiti hicho kiliwacha wazi kufuatia kifo cha seneta Haji kilichotokea katika hospitali ya Aga Khan Februari 15 mwaka huu.

Haji aligonga vichwa vya habari baada ya kuwanusuru Wakenya waliokuwa wamekwama kwenye jumba la West gate mwa kwa wa 2013.

Gavana wa Garissa Ali Korane alikua mstari wa mbele kumpigia debe Abdikadir na kuwasihi wakazi wa Garissa kumuunga mkono Haji.

Abdikadir huenda akachaguliwa bila kupingwa ikizingatiwa kwamba hana mpinzani kwa sasa. Akizungumza baada ya hafla hiyo Abdikadir amewashukuru wote walio fanikisha hafla hiyo.

"Hii ni hatua nyingine ambayo tunachukua leo. Wacha tutembee safari hii hadi tamati, kile nawaahidi ni kwamba nitakua mhudumu wenu" Alisema Abdikadir

Abdikadir alikua ameandamana na naibu Gavana abdi Dagane, Mbunge wa Ijara Sophia Abdi Noor na spika wa kaunti Mohammed Abbas

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke