Mon, 3 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 54 aliyefahamika kwa jina moja la Rusengamihigo kutoka nchini Rwanda, ameamua kuisaka elimu na kurejea darasani.
Mwanaume huyo amewashangaza wengi baada ya kuanza elimu ya msingi (Primary School) akiwa tayari ni mtu mzima.
Rusengamihigo alipokwenda Shuleni hapo kwa ajili ya usajili, yeye alipenda kuanzia darasa la tatu (3) ila Waalimu wa shule hiyo wakapendelea na kumshauri aanzie daraja la tano (5).
Baba huyo tayari ameanza shule licha ya changamoto anazokabiliana nazo akiwa na sare za shule pamoja na Wanafunzi wenzie kumshangaa kutokana na umri wake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live