Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanariadha Mkenya aliyetimuliwa kwenye Olimpiki kwa kutumia pufya, ajitetea

1581261937531d3e Mwanariadha Mkenya aliyetimuliwa kwenye Olimpiki kwa kutumia pufya, ajitetea

Sun, 1 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mark Otieno alipigwa marufuku akijiandaa kushiriki kwenye raundi ya kwanza ya mbio za mita 100 kwenye Tokyo Olympics Sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 28, zilionyesha alitumia dawa za kusisimua misuli huku timu ya Kenya ikikinzana na marufuku hayoKulingana na Otieno, hawezi kujishughulisha na mambo ambayo yatamuweka taabani pamoja na timu yake

Mtimkaji nyota wa Kenya, Mark Otieno ameapa kusafisha jina lake kufuatia kupigwa marufuku kwenye mashindano ya Tokyo Olympics kwa sababu ya kutumia dawa za kusisimua misuli.

Otieno alipigwa marufuku akijiandaa kushiriki kwenye raundi ya kwanza ya mbio za mita 100 kwenye Tokyo Olympics.

TUKO.co.ke imetambua kuwa haya ni baada ya sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 28, zilionyesha alitumia dawa za kusisimua misuli.

Otieno aliondolewa kwenye mbio za Jumamosi, Julai 31, ambapo alitarajiwa kukimbizana na Mkenya mwenzake Ferdinand Omanyala.

Read also

Didmus Barasa Akanusha Alimlima Kofi Steve: "Nilikuwa Namuashiria Afunge Zipu Yake"

Hata hivyo, mwanariadha huyo amesema hawezi kujishughulisha na mambo ambayo yatamuweka taabani pamoja na timu yake.

Katika taarifa kwenye kurasa zake za mtandao wa kijamii, Otieno aliahidi kuthibitisha kuwa hana hatia akiwa na matumiani ya kuendeleza taaluma yake.

"Uadilifu wangu kama mwanariadha ni muhimu kwangu, na nashukuru sana nafasi ambayo nimepewa kuwakilisha taifa langu kimataifa."

"Kwa hivyo siwezi kujihusisha na mambo ambayo yataniathiri pamoja na timu yangu. Bado nina matumaini ya kusafisha jina langu na kuendelea na safari yangu ya riadha," aliandika.

Inaaminika kuwa timu ya Kenya pia ilikinzana na marufuku hayo ikidai kuwa huenda kulikuwa na utata kwenye maabara.

Wizara ya Michezo kwa upande wake kupitia kwa Katibu Mkuu Joe Okudo, ilishikilia kuwa serikali inakaza kamba katika kukabiliana na matumizi ya dawa za kusisimua misuli.

“Wizara bado inasubiri rufaa iliyowasilishwa na mwanariadha huyo na kuhujumu juhudi za Serikali za kupigana na matumizi ya pufya."

“Mikakati muhimu kulingana na sheria ya mamlaka ya Kenya dhidi ya dawa za kusisimua misuli na sheria ya kimataifa, hatua zitachukuliwa dhidi ya mwanariadha punde baada ya taratibu kufuatwa na kukamilika," alisema Okudo.



Read also

Bungoma: Mganga Ahukumiwa Maisha kwa Kumpa Mteja Miti Shamba Yenye Sumu

Marufuku ya Otieno inakujia wakati timu ya Kenya inajiburuta kwenye mashindano ya Tokyo Olympics 2020 huku timu hiyo ikikosa kushinda medali yoyote.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke