Sun, 14 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shaden Gardood (37) ameuawa wakati mapigano ya kugombea Madaraka yakiendelea kati ya vikosi vya Jeshi la Sudan dhidi ya Rapid Support Forces (#RSF) katika Mji wa Omdurman, ikiwa ni Siku moja baada ya pande hizo kuafikiana kupunguza mapigano.
Gardood alikuwa mmoja wa Watu maarufu wanaopinga machafuko hayo na alirekodi video kadhaa kisha kuziweka Mtandaoni akielezea anavyopinga kinachoendelea Sudan
Zaidi ya Wananchi 600 wameuawa huku zaidi ya 4,000 wakijeruhiwa tangu kuanza kwa vita hiyo Aprili 2023, pia 80% ya Hospitali zina changamoto ya Chakula, Maji na umeme.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live