Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanamke wa Ethiopia miongini mwa watu saba walionyongwa nchini Kuwait

Hukumu Pc Data Mwanamke wa Ethiopia miongini mwa watu saba walionyongwa nchini Kuwait

Wed, 16 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kuwait imekeleza mauaji hukumu yake ya kwanza ya kifo katika kipindi cha miaka mitano, kunyongwa watu saba wakiwemo wanawake wawili licha ya maombi ya wanaharakati wa haki za kimataifa kutaka wahurumiwe.

Kulingana na idara ya mashtaka ya umma, waliouawa ni mwanamke kutoka Ethiopia na mwingine kutoka Kuwait, mwanamume wa Syria na Pakistani, na wanaume watatu wa Kuwait.

Kuwait imewanyonga karibu watu 80 tangu miaka ya 1960, wengi wao walikabiliwa na kesi za mauaji au dawa za kulevya.

Shirika la Amnesty International limeitaka nchi hiyo ya Ghuba kushinikizwa isitishe mauaji hayo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live