Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanamke aliyepigiwa simu ya maajabu usiku wa manane kufuata nyama, auawa

Mauaji Abc.jpeg Mwanamke aliyepigiwa simu ya maajabu usiku wa manane kufuata nyama, auawa

Fri, 10 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hali ya utulivu katika Wilaya ya Busia Mashariki mwa Uganda ilitatizwa na ugunduzi wa kutisha huku maiti ya mwanamke mwenye umri wa miaka 40 ikipatikana imetupwa River Solo mnamo Mei 8, 2024.

Tukio hilo limesababisha polisi kuanzisha uchunguzi wa haraka, huku watuhumiwa watatu wakiwa tayari wanazuiliwa. Kwa mujibu wa Moses Mugwe, Msemaji wa Polisi Mkoa wa Bukedi, mwili wa Paulina Lokiru uligunduliwa asubuhi, kama ilivyoripotiwa na Daily Monitor.

"Tulipokea taarifa zinazohusu mauaji ya mwanamke mwenye umri wa miaka 40 na tumewakamata watu watatu huku uchunguzi ukiendelea," alisema Mugwe.

Hata hivyo, sababu za mauaji hayo bado hazijaeleweka, na kuacha maswali mengi bila majibu. Jambo la kustaajabisha ambalo limeibuka ni simu ya ajabu iliyopokelewa na mwathiriwa mwendo wa saa saba usiku, ikimrubini kutoka katika makazi yake kwa kisingizio eti kulikuwa na nyama ya bure.

Polisi wanachunguza kwa kina ikiwa simu hii ilitekeleza jukumu muhimu katika kifo chake cha kusikitisha. Sam Mbogo, mwenyekiti wa LCI wa Kijiji cha Solo 'A', alisimulia jinsi wakazi walivyojikwaa na tukio hilo la huzuni wakati wakielekea kwenye mashamba yao asubuhi.

"Waliona damu kwenye ukingo wa mto, na walipokagua kwa karibu, waligundua mwili wake ukiwa kando ya mto," alifafanua Mbogo. Wenyeji walimkumbuka Lokiru kama mtu anayejali wengine ambaye alifanya kazi kwa bidii na mfanyabiashara wa nafaka katika soko kuu la Busia. Mumewe, Paul Agan, mlinzi, alieleza alipokuwa usiku huo wakati wa tukio hilo, akisema kuwa alikuwa zamu.

Agan alielezea kushtuliwa kwake na mkasa huo, akimtaja mkewe kama mtu ambaye "hajawahi kuwa na kinyongo na mtu yeyote,". Huku mamlaka ikiendelea kupembua ushahidi na jamii ikikabiliana na kifo cha kutisha cha mwanamke huyo uchunguzi ungali unaendelea.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live