Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanamke aliyeonekana akivuta mkokoteni awagusa wengi

Mama Mkokoteni Mwanamke aliyeonekana akivuta mkokoteni awagusa wengi

Fri, 24 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanamke Mkenya kutoka Dagorreti ambaye alipepea mitandaoni baada ya picha yake akivuta mkokoteni mzito amefariki dunia.

Everlyn Ndinyuki aliwasisimua Wakenya wengi baada ya picha yake kupepea mitandoani ambapo alionekana akifanya kazi kwa bidii ili aweze kuwahudumia watoto wake.

Mfadhili mashuhuri Wanja Mwaura ambaye aliwahimiza Wakenya kumwokoa kutoka kwa kazi ngumu mapema leo, alitangaza kuwa mwanamke huyo mchapakazi hayupo tena.

Katika mtandao wake wa kijamii, Wanja alisema Ndinyuki alifariki dunia Jumanne, Machi 21, baada ya kuugua kwa muda mfupi.

"Unamkumbuka mama Denno? (Everlyn Ndinyuka) Mwanmke mmoja aliyekuwa akivuta mkokoteni akiuza maji? Mnamo Julai 2021, tuliungana na kumfungulia duka la nafaka ili kumwondolea kazi hii ya sulubu.

Jana nilipata habari za kusikitisha kwamba alifariki dunia Jumanne usiku baada ya kuugua kwa muda mfupi. Bado hakuna mipango iliyofanywa ya kumzika. Tunawaombeautulivu, haswa watoto wake," Wanja alisema.

Msamaria Mwem Wanja Mwaura aliangazia kwa mara ya kwanza kisa cha mwanamke aliyetambuliwa kama Everlyn Ndinyuka mnamo Juni 10, 2021.

Kupitia Facebook, Wanja aliomba usaidizi wa kumtafuta mwanamke aliyeonekana akiwa amebeba mitungi ya maji kwenye mkokoteni huko Dagoretti.

Wanja alifaulu kumtafuta mwanamke huyo, na mnamo Juni 14, alimtembelea pamoja na watu wengine waliomtakia heri.

Kulingana na Wanja, Ndinyuka aliishi katika chumba kimoja na watoto watano. Wawili kati yao ni wana wa marehemu dadake, na mmoja ni mpwa wake.

Katika ziara hiyo, wasamaria wema waligundua kuwa kuvuta mkokoteni huo kumeathiri vibaya mwili wa Ndinyuka.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live