Mon, 29 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanajeshi Emmanuel Chakwanda amehukumiwa kifungo cha miaka kumi jela kwa kutishia kumshambulia Afisa wa Polisi anayesimamia usalama barabarani (trafiki) huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Uamuzi wa Mahakama ya Kijeshi ya Ngaliema mjini Kinshasa ulitolewa baada ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikimuonyesha askari huyo akimnyooshea afisa wa Polisi silaha yake na kufyatua risasi hewani.
Watu wamelaani mwenendo wa askari huyo bila kusahau mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini humo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live