Thu, 23 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kapteni Paul Rukaria, amefungua mashtaka dhidi ya Rais William Ruto na Mwanasheria Mkuu wa Serikali akipinga kutenguliwa Uenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Kitaifa la Biashara la Kenya (KNTC).
Rukaria amedai kuwa Rais hakushauriana na Kamati ya Ushauri ya Mashirika ya Serikali kabla ya kutengua uteuzi wake na hivyo anaiomba Mahakama isimamishe uteuzi wa Mwenyekiti mpya na kumrejesha yeye.
Afisa huyo wa Jeshi aliteuliwa na Rais wa Mstaafu Uhuru Kenyatta Agosti 5, 2022 kwa Utmishi wa miaka 3 zikibakia siku 4 kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Nchi hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live