Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanaharakati aliyeachiliwa kwa dhamana ya KSh 500k achangiwa na Wakenya

De79b0c260feb878 Mwanaharakati aliyeachiliwa kwa dhamana ya KSh 500k achangiwa na Wakenya

Thu, 8 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kiama aliachiliwa kwa dhamana baada ya Hakimu Kamau kusema haoni sababu ya kumzuia kwa siku 14 kulingana na ombi la polisi

- Wanaharakati wenzake na Wakenya wengine mitandaoni kwa sasa wanaendesha mchango ili kumsaidia kulipa hela hizo

- Ameamriwa ajiwasilishe katika kituo cha polisi cha Central kila siku kwa siku kumi zijazo

Wanaharakati wa Kenya wameungana kumsaidia mmoja wao, Edwin Kiama, ambaye alikamatwa kwa madai ya uhalifu wa kimtandao.

Mnamo Jumanne, Aprili 6, mwanaharakati huyo alikamatwa kufuatia mabango aliyobuni kumdhihaki Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto kuhusu Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).

Mwanaharakati huyo alizuiliwa kwa siku mbili.

Aliwasilishwa Alhamisi, Aprili 8, mbele ya Hakimu Mwandamizi Jane Kamau katika Mahakama ya Milimani, ambapo alipewa dhamana ya Ksh 500,000 pesa taslimu.

Ili kuonesha kuwa wanasimama naye, Wakenya mitandaoni wakiongozwa na wanaharakati wenzake walianzisha kampeni ya kuchaga pesa kumsaidia mwanaharakati huyo kulipa dhamana hiyo.

Mbali na dhamana hiyo, mwanaharakati huyo aliamriwa kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Nairobi Central kila siku hadi Aprili 18. Aliagizwa piwa kutochaopisha lolote kwenye kurasa zake za mitandao ya jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kiama alisema kuwa hajutii picha za alizopakia mitandaoni ambazo zilimtia taabani.

Mwanaharakati huyo alisema kwamba alikuwa ametenda kulingana na uhuru wa kujieleza uliomo kwenye Katiba.

Mabango yake yalionekana kuchovhea hasira miomgoni mwa Wakenya kufuatia mkopo wa KSh 257 bilioni kwa Kenya kutoka IMF.

Katika mabango yake ambayo yalikuwa na picha za Uhuru na Ruto, Kiama alionya IMF na wapeanaji wengine dhidi ya kutoa mikopo kwa Kenya.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke