- Kiama aliachiliwa kwa dhamana baada ya Hakimu Kamau kusema haoni sababu ya kumzuia kwa siku 14 kulingana na ombi la polisi
- Wanaharakati wenzake na Wakenya wengine mitandaoni kwa sasa wanaendesha mchango ili kumsaidia kulipa hela hizo
- Ameamriwa ajiwasilishe katika kituo cha polisi cha Central kila siku kwa siku kumi zijazo
Wanaharakati wa Kenya wameungana kumsaidia mmoja wao, Edwin Kiama, ambaye alikamatwa kwa madai ya uhalifu wa kimtandao.
Mnamo Jumanne, Aprili 6, mwanaharakati huyo alikamatwa kufuatia mabango aliyobuni kumdhihaki Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto kuhusu Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).
Aliwasilishwa Alhamisi, Aprili 8, mbele ya Hakimu Mwandamizi Jane Kamau katika Mahakama ya Milimani, ambapo alipewa dhamana ya Ksh 500,000 pesa taslimu.
Ili kuonesha kuwa wanasimama naye, Wakenya mitandaoni wakiongozwa na wanaharakati wenzake walianzisha kampeni ya kuchaga pesa kumsaidia mwanaharakati huyo kulipa dhamana hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kiama alisema kuwa hajutii picha za alizopakia mitandaoni ambazo zilimtia taabani.
Mwanaharakati huyo alisema kwamba alikuwa ametenda kulingana na uhuru wa kujieleza uliomo kwenye Katiba.
Mabango yake yalionekana kuchovhea hasira miomgoni mwa Wakenya kufuatia mkopo wa KSh 257 bilioni kwa Kenya kutoka IMF.
Katika mabango yake ambayo yalikuwa na picha za Uhuru na Ruto, Kiama alionya IMF na wapeanaji wengine dhidi ya kutoa mikopo kwa Kenya.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.