Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanahabari Lofty Matambo aagana na KTN baada ya kuhudumu miaka 7

14a406c2d61e5c93 Mwanahabari Lofty Matambo aagana na KTN baada ya kuhudumu miaka 7

Mon, 19 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Lofty Matambo aliwaaga mashabiki wake huku akisoma habari zake za mwisho Jumapili jioni

- Mtangazaji huyo wa lugha ya Kiswahili aliwashukuru watazamaji wake kwa kumuonyesha upendo wao kwenye runinga na radio

- Lofty pia alishukuru shirika la Standard Group kwa nafasi waliomupa na wafanyakazi wenzake

Mwanahabari wa lugha ya Kiswahili Lofty Matambo ameagana na KTN na shirika la Standard Group baada ya kuhudumu kwa miaka saba.

Lofty Matambo aliwaaga mashabiki wake huku akisoma habari zake za mwisho kituoni humo siku ya Jumapili,Aprili 18 jioni.

Mwanahabari huyo alisema alijiunga na KTN akiwa limbukeni lakini aliendelea kujinawirisha.

Aliwashukuru mashabiki wake kwa kumuonyesha upendo kwenye runinga na pia Radio Maisha ambapo pia alikuwa na shoo yake na ilikuwa vigumu kuwaaga.

Lofty pia alishukuru shirika la Standard Group kwa nafasi waliomupa na wafanyakazi wenzake .

"Mashabiki wangu nyinyi ni wa thamini kama dhahabu, wacha tuendelee kuthaminiana hata huko nje na tutakutana tena," aliongezea.



Hakufichua atajiunga na kituo kipi ama kama endapo ataendelea kuwa msomaji wa habari.

Kulingana na duru za kuaminika zilizozungumza na TUKO.co.ke, tayari Lofty alikuwa anapania kujiunga na NTV.

KTN imewapoteza wanahabari wake wawili mahiri wa lugha ya Kiswahili baada ya mwanahabari Fridah Mwaka kuondoka.

Mrembo huyo alitangaza habari kwa mara ya mwisho Jumapili, Machi 21.

Siku chache zilizopita, Mwaka alifichua kuwa aliwacha kazi yake ili kufuata ndoto yake ya mapishi na mavazi.

"Kando na fasheni, nina biashara ya chakula kwa jina Vidoho food, ambapo huwa ninapika na kusambaza chakula eneo la Pwani kwa wateja," Mwaka aliambia TUKO.co.ke.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke