Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanafunzi wa miaka 15 azunguka jijini na bango akiomba ada ya shule

91f78e06325e9350 Mwanafunzi wa miaka 15 azunguka jijini na bango akiomba ada ya shule

Thu, 16 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mellan Njeri, mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Kihumbu-ini katika kaunti ya Murang'a alilazimika kuzunguka katika barabara za jijini akiomba karo ya shule.

Mwanafunzi wa kidato cha pili Mellan Njeri alilazimika kuzunguka mjini alasiri na bango la kuwasihi wasamaria wema kumsaidia na karo ya shule.

Akiwa amevalia sare ya shule, mwanafunzi huyo alizunguka katika barabara za jijiji akitarajia kuchangisha KSh 29,000 zinazohitajika shuleni Hata hivyo, jitihada zake hazikulipa kwani kufukia saa saba na dakika 45 alikuwa amepata tu KSh 500

Ili kuwavutia wasamaria wema, Njeri alizunguka katikati mwa jiji la Nairobi akiwa amebea bango lenye ujumbe "naomba nisaidie na karo ya shule."

The Standard iliripoti kuwa mwanafunzi huyo alitumwa nyumbani kutokana na malimbikizo ya KSh 29,177.

Ripoti zilionesha kuwa kufikia saa saba na dakika arobaini na tano, mwanafunzi huyo na rafiki yake Mary Wanjiru walikuwa wamezunguka barabara za Lang'ata, parliament, Professional Way, Kenyatta Avenue lakini walikuwa wamefanikiwa kuchanga tu KSh 500.



"Ni rafiki yangu na jirani na ndio maana niliandamana naye kwani namjua na naijua familia yake," rafiki yake Njeri alisema.

Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 15 ambaye alikuwa amevaa sare rasmi ya shule, alielezea kwamba alifukuzwa shule kutokana na malimbikizo mnamo Septemba 10 lakini mamake hakuwa na uwezo wa kupata hela hizo.

Ni kutokana na hali hii ambapo aliomba msaada kwa umma kwani mtihani wake wa kukamilisha muhula utafanyika katika juma moja lijalo.

Mamake Anne Wangechi Mureithi alithibitisha hadithi hiyo, akiongeza kuwa anatafuta lishe kupitia vibaraua kwani ni yeye pekee mlezi wa Njeri na ndugu zake wengine watatu.

"Amekuwa akifukuzwa shuleni mara kwa mara na alipofika nyumbani mnamo Septemba 10, sikuwa na njia nyingine na ndiyo maana tuliamua kuandika ujumbe kwenye bango kisha tukamruhusu kusafiri kutoka Ruiru kwenda Nairobi," mama huyo alielezea.

Wakati shule yake ilipopigiwa simu katibu alikiri kwamba taasisi hiyo inafahamu kisa cha Njeri ila mamake bado hajafika shuleni humo kuzungumza na usimamizi.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke