Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanafunzi auawa kwa kukashifu dini

Moto Mauaji Mwanafunzi auawa kwa kukashifu dini

Fri, 13 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ghasia zimezuka katika chuo cha elimu ya juu katika mji wa Sokoto kaskazini mwa Nigeria baada ya mwanafunzi wa kike wa Kikristo kudaiwa kutoa matamshi ya kashfa dhidi ya Uislamu.

Eneo hilo lina Waislamu wengi.

Wanafunzi wa Kiislamu katika Chuo cha Elimu cha Shehu Shagari wanaripotiwa kumuua msichana huyo na kuuchoma moto mwili wake.

Kisha wakaingia kwenye msako wa kuharibu mali yakiwemo magari.

Msemaji wa polisi katika jimbo la Sokoto aliambia BBC kuwa vikosi vya usalama viliingilia kati kurejesha hali ya utulivu na uchunguzi unaendelea.

Mamlaka imekifunga chuo hicho kwa muda usiojulikana na kuwaamuru wanafunzi kurudi nyumbani mara moja.

Kiongozi mkuu wa kidini wa Kiislamu nchini Nigeria, Sultan wa Sokoto, Sa'ad Abubakar, amelaani mauaji ya mwanafunzi huyo wa Kikristo na kuomba utulivu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live