Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwalimu Mkuu awafungia nje walimu kwa kufika shuleni wakiwa wamechelewa

909180331778a987 Mwalimu Mkuu awafungia nje walimu kwa kufika shuleni wakiwa wamechelewa

Wed, 28 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Baadhi ya walimu katika Shule ya Msingi ya Sichekhe walifedheheshwa na kufungiwa nje ya taasisi hiyo kwa kufika wakiwa wamechelewaMwalimu Mkuu, George Bwire alisema ni vigumu kwa walimu hao kujipanga katika masomo yao ikiwa watafika shuleni wakiwa wamechelewaWalimu hao walioonekana kutofurahishwa na walichotendewa, walaimtaka mwalimu mkuu huyo kuwaheshimuKatika Shule ya Msingi ya Sichekhe eneo la Namboboto kaunti ya Busia sheria ya kufika shule mapema haimsazi yeyote kuanizia kwa walimu hadi wanafunzi.

Mnamo Jumatatu, Julai 27 walimu katika taasisi hiyo walipigwa na butwaa baada ya kufungiwa nje ya lango la shule hiyo kwa kufika wakiwa wamechelewa.

Katika taarifa ya NTV, walimu hao walijikuta katika njia panda na wale ambao hawakutaka kukosa kutekeleza kazi yao walilazimika kupenyeza hadi shuleni humo kupitia kwenye ua.

Mwalimu Mku, George Bwire alisema ni vigumu kwa walimu kujipanga katika masomo yao ikiwa watafika shuleni wakiwa wamechelewa

Alisema kila mmoja alipaswa kuzingatia wakati ikiambatana na masuala ya elimu.



Read also

Magazeti Ijumaa: Moses Kuria Afukuzwa PEP, UDA Yakumbwa na Mzozo

"Nimebaini kwamba walimu wanafika shuleni saa mbili na dakika ishirini asubuhi na huo ndio wakati ambao wanapaswa kuwa wanajipanga kuanza kufunza," Bwire alisema.

Wakiwa wameudhika na tukio hilo, walimu hao walilalamika jinsi ambavyo wamefedheheshwa mbele ya wanafunzi ambao waliwacheka wakidhani mwalimu mkuu atawatandika.

"Hatuna hata raha ya kufanya kazi tena sababu kila unapoingia tu katika lango la shule, wanafunzi wanaanza kukuchekelea wakidhani kwamba pia sisi tutatandikwa na mwalimu mkuu kwa kufika shuleni tukiwa tumechelewa," mwalimu huyo alisema.

Wakati uo huo alimtaka mwalimu mkuu huyo kuwaheshimu.

Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari walifungua shule siku ya Jumatatu kwa muhula wao wa kwanza katika kalenda ya masomo ya 2021/2022.

Muhula wa kwanza ulianza Julai 26 hadi Oktoba 1, 2021.

Muhula wa pili utaanza Oktoba 11, 2021, hadi Desemba 23, 2021, na baada ya hapo wanafunzi wataripoti shuleni kwa muhula wa 3 Januari 3, 2022, hadi Machi 4 , 2022.



Read also

Picha ya Mbwa Waliohudhuria Mazishi na Kuomboleza Yazua Mdahalo

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke