Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mvunja mbavu mkongwe Nyambane atangaza kuwania urais 2022

Bf6f7dd65701156f Mvunja mbavu mkongwe Nyambane atangaza kuwania urais 2022

Tue, 27 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Nyambane alipata umaarufu kupitia kipindi cha kuvunja mbavu, Redykyulass

- Alisema ndoto yake ya kuwa rais ilichochewa na kumuiga rais wa zamani Daniel Moi kwenye shoo hiyo

- Mong'are pia alielezea sababu ya kuwacha kutumia jina lake la usanii 'Nyambane' baada ya kuteuliwa mkurugenzi wa masuala ya vijana

Mkurugenzi wa Masuala ya Vijana,Walter Mong’are almaarufu Nyambane ametangaza kuwa atawania urais wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Nyambane ambaye alipata umaarufu kupitia kipindi cha kuvunja mbavu Redykyulass, alisema ndoto yake ya kuwa rais ilichochewa na kumuiga rais wa zamani Daniel Moi kwenye shoo hiyo.

Mongare alifichua haya wakati wa mahojiano na mchekeshaji mwenzake Daniel Ndambuki almaarufu Churchill, Jumapili, Aprili 25.

“Nilikuwa nikiwaiga marais na wajua waeza kuiga kitu hadi uwe ma ninaamini itatimia siku moja. Rais wangu anafahamu kile kinaendelea."

"Uchaguzi unakuja 2022 na rais wetu alifanya kile aliweza kwa uwezo wake kwa hivyo tunakuja 2022.Tunawapa Wakenya fursa wa kuchagua mtu mwingine kuendelea. Na wakati huu sijui ni nani atakuwa rais lakini siwezi jiweka nje. Ndoto hutimia," alisema.

Mong'are pia alielezea sababu ya kuwacha kutumia jina lake la usanii 'Nyambane' baada ya kuteuliwa mkurugenzi wa masuala ya vijana.

Alitaja hadithi ya Abrahamu kwenye bibilia ambaye Mungu alibadilisha jina lake ili amubariki.

Kwingineko kwenye taarifa ya ulingo wa uchekeshaji na siasa, mchekeshaji Jalang'o amepuzilia mbali mabango yanayosambaa mitandaoni yakionyesha kuwa anajipigia kampeni kisiasa katika uchaguzi mkuu ujao.

Mvunja mbavu huyo amekuwa akidokezea hatua ya kujiunga na siasa na huku mwaka 2022 ukikaribia, gumzo hilo limeibuliwa tena.

Jalang'o alipakia mtandaoni bango maridadi ambalo lilikuwa na jina lake kamili Felix Oduor na kuonyesha atawania ubunge 2022.

Bango hilo pia lilionyesha kuwa atawania kiti hicho kupitia tikiti ya Chama cha Amani National Congress (ANC).

Aliwaomba wafuasi wake kupuuza tangazo hilo akidai kuwa tayari watu wameanza kuwa na wasiwasi na bado hajatangaza hatua yake nyingine.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke