Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mvunja mbavu Mganda Anne Kansiime atarajia mwanawe wa kwanza

E3f41f67aa9c2b81 Mvunja mbavu Mganda Anne Kansiime atarajia mwanawe wa kwanza

Thu, 15 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mchekeshaji Anne Kansiime ana ujauzito wa mwanawe wa kwanza

- Kansiime na mpenzi wake Sky walianza kuchumbiana mwaka 2018 baada ya kutengana na mume wake wa zamani Gerald Ojuok mwaka 2017

- Tayari tumbo lake linachomoza ishara kwamba anatarajia kumbeba mwanawe hivi karibuni

Mchekeshaji tajika kutoka Uganda Anne Kansiime na mpenzi wake Skyla wanatarajia kupata mwanao wa kwanza.

Kansiime na mpenzi wake Sky walianza kuchumbiana mwaka 2018 baada ya kutengana na mume wake wa zamani Gerald Ojuok mwaka 2017.Wawili hao walikuwa wameishi pamoja kwa miaka minne.

Nyota huyo alisema ndoa yake ilivunjika kwa sababu ya kuharakisha kuolewa na Gerald Ojok.

"Mpango wangu ulikuwa kusoma na kufuzu, kupata kazi na kisha kuolewa. Lakini haikuwa hivyo," alisema.

Kansiime alitangza habari hizo njema kwenye mtandao wa kijanii, akiahidi kusimulia safari yake ya uja uzito Ijumaa.

"Nimekuwa nikitafuta njia mwafaka ya kutangaza habari hizi kwa wapendwa wangu Ninjas kuwa mpenzi wangu Kantu @skylantagramn a mimi tunatarajia kupata Ninja mdogo na nilifikiria sana ni njia ipi nitatumia?"alimaka.

Kansiime na mpenzi wake walikuwa wameficha habari hizo kuwa siri.

Wafuasi wake wamemupa kongole huku wakimsubiri malaika huyo.

Hii hapa maoni yao:

Patrick Salvado: "Skylanta Kansiime Anne nawafurahia sana watu wangu"

Bugingo Hannington: "Baraka tele dada yangu. Mungu wetu ni mwaminifu!Nawafurahia nyinyi nyote."

Akotheekenya alisema: "Hongera mama. Hii ni Mungu tu kila kitu nzuri huja kwa wakati

contactmakeda : "Amen! Mungu akubariki pamoja na familia yako! Hongera mama Kansiime Anne!."

wambulwaannette: "Mungu wangu, watu wangu wapendwa watakuwa na mtoto, Siwezi kujizuia banange.Hongera."

lydear aliandika: "Nimekuwa nashangaa umepotelea wapi Hongera kwako kwa baraka hiyo kubwa"

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke