Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Muungane au DP Ruto awachape asubuhi mapema, Ngilu awaambia Raila na Kalonzo

4df85ac090e53867 Muungane au DP Ruto awachape asubuhi mapema, Ngilu awaambia Raila na Kalonzo

Sat, 12 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ngilu alisema kura za Wakamba zitapotea iwapo Kalonzo hataungana na Raila kwenye safari ya Ikulu

- Alisema wasipofanya muungano DP atawashinda asubuhi na mapema kwenye kinyang'anyiro cha Ikulu

- Wawili hao walitakiwa kuunda muungano kama alioongoza Raila 2002 uliompeleka Moi nyumbani

Naibu Rais William Ruto atashinda uchaguzi asubuhi na mapema 2022 iwapo Raila Odinga na Kalonzo Musyoka hawataungana, Gavana Charity Ngilu amesema.

Ngilu aliwakumbusha wawili hao kuhusu urafiki wao 2013 ambapo walikuwa na ufuasi mkubwa kwenye safari ya kuingia Ikulu.

Aliwataka kupanga karata kama waliyopanga 2002 wakati wa Kanu na wakafaulu kumtuma nyumbani Daniel Moi na chama chake.

Nitajaribu nione kama naweza kuwaleta pamoja. Kalonzo wewe uko sawa kuwa rais, lakini tunapoteza wakati na hakuna saa. Mketi chini muuongee kimoja. Mheshimiwa Raila Odinga, wewe na Kalonzo, kama mlivyofanya 2002," alisema Ngilu.



Ngilu alisema Ukambani inaendelea kuachwa nyuma katika minofu ya serikali ambayo inagawiwa maeneo mbali mbali.

Alimtaka Raila kutetea eneo hilo ili liweze kupata mgao kama vile Kisumu ilivyofaidika na miradi ya serikali kutokana na handisheki.

"Tafadhali ni lazima tukae chini ili ata sisi ukambani tuletewe kitu. Ata sisi tuko ndani ya handisheki," alisema Ngilu.

Raila alisema yuko tayari kufanya kazi na Kalonzo ili kuingia Ikulu 2022 akiashiria kuna mipango inayoendelea faraghani.

"Mimi na Kalonzo hatuwezi kukosana. Tutakubaliana tu . . . tutasimama pamoja ili tuweze kutoa hawa wezi ambao wanadanganya Wakenya. Mimi bnataka Wakenya wasimame imara," alisema Baba.

Raila aliwakashifu baadhi ya viongozi wa kanisa kwa kusherekea maamuzi ya Mahakama ya Juu kusimamisha reggae ya BBI.

"Nyinyi watu wa kanisa muwachane na sisi tuendeshe mambo ya siasa, apana kusema eti reggae ilisimama . . . nobody can stop reggae, wewe endelea na mambo yako ya kanisa huko," alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke