Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Museveni ashinda urais Uganda

Db2ee5b064d21e4699b4a53350b91a2f Museveni ashinda urais Uganda

Sun, 17 Jan 2021 Chanzo: habarileo.co.tz

Mgombea wa urais wa Uganda kupitia chama cha ‘National Resistance Movement’ Yoweri Museveni ametangazwa kuwa mshindi wa nafasi hiyo baada ya kupata kura 5,851,037 ambazo sawa na 58.64% ya kura zote zilizopigwa.

VIDEO >>> Museveni vs Bobi Wine: Mambo matatu kuhusu Uchaguzi Mkuu Uganda

Mpinzani mkuu wa Museveni katika kinyang’anyiro hicho Robert Kyagulanyi maarufu kama ‘Bob Wine’ ameshika nafasi ya pili kwa idadi ya kura 3,475,398 sawa na 34.83% ya kura zote zilizopigwa.

Uganda ilifanya uchaguzi Alhamisi tarehe 14, Januari 2021 na umefikia tamati hii leo mara baada ya Museveni kutangwaza mshindi wa kiti cha urais.

Ushindi huo unamaanisha kuwa Museveni ataendelea kuliongoza Taifa la Uganda kwa muhula mwingine baada ya kukaa madarakani kwa miaka 35.

Chanzo: habarileo.co.tz