Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuna haja ya kuwakamata raia wa taifa hilo wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya.
Akizungumza na vyombo vya habari rais huyo ameshutumu wale wanaosambaza habari kwenye mitandao kwamba yeye amefariki dunia.
Amesema kwamba wale wanaohusika na habari kama hizo wanapaswa kusakwa na kukamatwa kwa kuwa wamekuwa wakipotezea watu muda wao.
Alisema: Tatizo jingine ambalo linapaswa kutatutiliwa ambalo sio la kiusalama bali la kijinga ni mitandao ya kijami. Mitandao ya kijami imekuwa ikisema kwamba museveni amefariki. Hivyobasi naitaka idara ya usalama kusuluhisha tatizo hilo.
We need to crack down on the people that are misemploying social media, including the Ugandans abroad. Many are now using it to spread baseless and tasteless news with total abandon. I call upon security to look into this. It must be stopped, get these people. pic.twitter.com/OmIjqEYhTs
— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) July 8, 2021
Share this:TweetWhatsApp Related