Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mungu Msaidie Rais: DP Ruto aomba Mungu kumsaidia Rais Uhuru

Ab58c49a88d7adfc Mungu Msaidie Rais: DP Ruto aomba Mungu kumsaidia Rais Uhuru

Fri, 20 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ruto amefanya maombi akiomba Mungu kuwapa hekima viongozi wa Kenya ili kuendesha nchi kwa njia ifaayoRuto na Rais wamekosana kisiasa na sasa serikali ni kama imegawanyika huku kila mmoja akiunda kambi na wandani wake.

Ruto amekuwa akitumia kanisa kama ngao yake siasa huku akisema ana imani Mwenyezi Mungu atampa nguvu ya kukabiliana na mahasimu wakeVideo imeibuka mtandaoni ambapo Naibu Rais William Ruto anaskika akimuombea Rais Uhuru Kenyatta kupata hekima ya kuongoza taifa.

Kwenye video hiyo, DP anasema ni mkono wa Bwana pekee ambao utawasaidia viongozi kuweza kuiongoza nchi.

Alisema Kenyatta anahitaji hekima na uongozi kutoka binguni ili Kenya iweze kusonga mbele.

"Mungu tunaombea uongozi wa Kenya, tunaombea Rais wa Jamhuri ya Kenya kuwa ukampe hekima na kumuongoza ili atekeleze mamlaka kama utakavyo.

Na sisi ambao tuko chini yake tunaomba utupe nafasi ya kuhudumu na tuwe baraka kwa nchi hii," alisema Ruto.



DP na Rais wamekuwa na tofauti kali za kisiasa kiwango cha kuwa sasa Ikulu inampigia debe kinara wa ODM Raila Odinga kuchukua usukani baada ya Kenyatta kuondoka.



Wawili hao wamekuwa na urafiki mkubwa tangu 2013 lakini mambo yalibadilika 2017 Rais alipoingia Ikulu kwa kipindi cha pili.

Mkataba wa handisheki kati ya Raila na Uhuru ndio ulikuwa kama msumari kwenye kidonda na sasa DP amesalia kulia na kusaga meno akisema serikali aliyosaidia kuunda inamfinya.



Ruto amekuwa akitumia kanisa kama ngao yake siasa huku akisema ana imani Mwenyezi Mungu atampa nguvu ya kukabiliana na mahasimu wake.

Amekuwa akisema kuwa wapinzani wake ni watu wenye mizizi ya kifamilia na kuwa na marafiki wenye ushawishi lakini yeye ako na 'God the Father'.

Amekuwa akikashifiwa kwa madai ya kutumia jukwaa kanisani kurindima siasa za urais 2022 kila anapofika ingia kuabudu.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke