Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mudavadi atagombea 2022 licha ya kuwepo mazungumzo

5871cde62a06e7ff Mudavadi atagombea 2022 licha ya kuwepo mazungumzo

Wed, 11 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Seneta Cleophas Malala amesisitiza kwamba Musalia Mudavadi ndiye kiongozi bora kuchukua uongozi wa taifa hili baada ya uchaguzi wa 2022Madai ya Malala iliashiria kwamba Mudavadi anaazimia kuwania urais licha ya vigogo wa Muungano wa OKA kufanya mazungumzo mjini Mombasa Agosti 10Rais Uhuru Kenyatta aliwataka vigogo hao kuungana tena kabla ya uchaguzi mkuu wa 2022Seneta wa Kakamega Cleophas Malala amesema kwamba Kiongozi wa chama cha ANC Musalia Mudavadi ndiye mgombea tosha wa urais katika uchaguzi mkuu wa 2022.

Malala alisisitiza kwamba Mudavadi ana uwezo na ujuzi wa kuliongoza taifa hili ikizingatiwa kwamba amekuwa serikalini kwa miaka mingi na anaelewa pia siasa.

" Mheshimiwa Musalia Mudavadi atafanya kila awezalo kuingia ikulu ifikapo 2022. Kutoka Mombasa hadi katika sehemu zingine za nchi, chama cha ANC kiko tayari kuchukua uongozi wa nchi hii," Malala alisema.

Madai ya Malala yanajiri saa chache baada vinara wa OKA akiwemo Musalia Mudavadi, Moses Wetangula, Kalonzo Musyoka na Gideon Moi kufanya mazungumzo ya kufanya kazi kwa pamoja mjini Mombasa.



Read also

Magazeti ya Jumatano, Agosti 11: Wandani wa Ruto Kupigwa Shoka Katika Baraza la Mawaziri

Vinara hao walifanya mkutano huo Jumanne, Agosti 10 na Rais Uhuru Kenyatta katika ikulu ya Mombasa, walijadili masuala kadhaa ikiwemo jinsi ya kufufua uchumi wa nchi.

Kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga pia alikuwa kwenye mkutano huo.

" Kati ya masuala yaliojadiliwa na viongozi hao ni athari za ugonjwa wa COVID-19 kwa taifa na jinsi ya kufufua uchumi, umuhimu wa kudumisha amani na umoja," Taarifa ya ikulu ilisoma.

Hata hivyo, vinara hao pia wanasemekana kujadili kuhusu siasa za mwaka wa 2022.

Awali Uhuru alitangaza kwamba atamuunga mkono kinara mmoja wa NASA katika uchaguzi wa 2022 iwapo wataafikiana kufanya kazi kwa pamoja.

Haijabainika wazi iwapo Raila atawania tena urais lakini kumekuwa na fununu kwamba atapeperusha bendera ya chama cha ODM.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke