Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mudavadi apuuzilia mkutano wa Raila, Gideon na Muhoho uliofanyika Karen

927d204a19d888a0 Mudavadi apuuzilia mkutano wa Raila, Gideon na Muhoho uliofanyika Karen

Thu, 15 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mudavadi amewaka Wakenya kukoma kuchambua kila hatua ya wanasiasa kwa mujibu wa uchaguzi ujao

- Alisema kuna uwezekano Raila, Gideon na Muhoho walikuwa wakijadili kuhusu mahari ya watoto wao walipokutana Jumanne Aprili 13

- Ni kikao ambacho kilizua hisia mseto kutoka kwa wadadisi wakisema kuna karata kubwa inachezwa

Kikao cha kinara wa ODM Raila Odinga, Seneta Gideon Moi na Muhoho Kenyatta nyumbani kwake Jumanne Aprili 13 kinazidi kuzua maoni tofauti.

Watatu hao ni kutoka familia tajika za kisiasa humu nchini na kikao chao kilichambuliwa kwa mirengo ya kisiasa na Wakenya.

Hata hivyo kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi amesema Wakenya sasa wamezidi na ni kosa kwa kila kitu kuangaliwa kwa jicho la kisiasa.

Mudavadi, ambaye yuko kwenye muungano wa One Kenya Alliance pamoja na Gideon Moi na Kalonzo Musyoka, alisema huenda watatu hao walikuwa na ajenda tofauti na siasa.

Akiongea na runinga ya Citizen, Mudavadi alisema muungano wao uko imara na hatua ya Gideon kukutana na Raila haijazua tumbo joto kwao.

"Watu sasa wamezidi kuhusu nani anafaa kukutana na nani. Walikuwa wanasema nini . . . labda walikuwa wakijadili mahari, labda watoto wao wantaka kuoana," Mudavadi aliambia Citizen.

Wadidisi walisema wanasiasa kama Muhoho, Gideon na Raila wanapokutana lazima kuwe na karata kali ya siasa ambayo inapangwa.

Kumekuwa na ripoti kuwa familia ya Kenyatta inapanga kumuunga mkono Gideon kuwania urais kwenye uchaguzi ujao kama njia ya kulipa deni la Mzee Daniel Moi la 2002.

Wakati huo, Moi alimchagua Uhuru Kenyatta kama mrithi wake na akatumia utajiri wake na ushawishi serikalini kumpigia debe.

Kenyatta hukiri kuwa ni hatua hiyo ya Moi ambayo ilimfanya kufaulu kwenye urais 2013 alipojaribu kwa mara ya pili.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke