Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mudavadi, Kalonzo na Wetang'ula wahama rasmi katika muungano wa NASA

4deaf3173b51aa6c Mudavadi, Kalonzo na Wetang'ula wahama rasmi katika muungano wa NASA

Tue, 3 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Muungano wa NASA uliundwa 2017 ambapo vyama vya ODDM, Wiper, Ford Kenya na ANC viliungana pamojaMuungano huo ulimpa kinara wa ODM Raila Odinga nafasi ya kupeperusha bendera ya uraisMudavadi, Wetang'ula na Kalonzo walisema walitafakari kuhusu malengo ya NASA na kuhisi kwamba hayawezi kuwafaidi tena katika siasa zaoMnamo Alhamisi, Julai 29 baraza la ODM lilisema limefanya uamuzi wa kugura muungano wa NASA kujipanga kutafuta narafiki wapya wa siasaMuungano wa National Super Alliance (NASA) ulioundwa kama chama cha Upinzani wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2017 umevunjwa rasmi.

Si ajabu kuwa muungano huo umefutiliwa mbali kwani vigogo wake wamekuwa wakivutana huku kila mmoja wa viongozi wake akitaka chama chake kipewe fursa ya mgombea wa kuwania urais 2022.

Wakati wa mkutano na waandishi wa habari Jumanne, Julai 3, kiongozi wa Amani National Congress Musalia Mudavadi, mwenzake wa Ford Kenya Moses Wetang'ula na Kalonzo Musyoka wa Wiper walitangaza kujiondoa kwenye muungano wa NASA.



Read also

Magazeti Jumatatu, Agosti 2: Raila Adokeza Kuungana Tena na Kalonzo, Mudavadi, Wetangula

Watatu hao walibaini kuwa walikuwa wamechunguza kwa uangalifu malengo na mafanikio ya umoja huo hayangewafaidi wananchi.

Mnamo Alhamisi, Julai 29 baraza la ODM lilisema limefanya uamuzi wa kugura muungano wa NASA kujipanga kutafuta narafiki wapya wa siasa.

"Bado tunashikilia kwamba NASA imepitwa na wakati. Ili kudhihirisha zaidi ukweli huu, Kamati ya Utendaji ya Kitaifa (NEC) ya ODM leo imeamua kuhama NASA," ilisema taarifa iliyosomwa na katibu mkuu wa chama hicho Edwin Sifuna.

Bado tunashikilia kwamba NASA imepitwa na wakati. Ili kudhihirisha zaidi ukweli huu, Kamati ya Utendaji ya Kitaifa (NEC) ya ODM leo imeamua kuhama NASA," ilisema taarifa iliyosomwa na katibu mkuu wa chama hicho Edwin Sifuna.

Muungano wa NASA umekabiliwa na changamoto tangu 2018 kutokana na kutokuaminiana kati ya vyama Wiper Democratic Movement, ODM, ANC na Ford Kenya.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.



Read also

Raila Amefanya Uamuzi wa Busara Kutema NASA - Moses Kuria Asema

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke