Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtuhumiwa mauaji Marekani atoroka jela Kenya

Sdfse Maujii Mtuhumiwa mauaji Marekani atoroka jela Kenya

Thu, 8 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mkuu wa polisi jijini Nairobi, Adamson Bungei, alisema Kevin Adam Kinyanjui Kangethe alitoroka katika kituo cha polisi na kuingia katika gari ndogo la kibinafsi na kwamba polisi ilikuwa inafanya operesheni ya kumsaka.

Polisi wanne waliokuwa zamuni katika kituo hicho walitiwa mbaroni na wameandikisha taarifa kuhusiana na tukio hilo.

Maafisa hao walisema kuwa mwendo wa saa 10:00 jioni ya Jumatano (Februari 7), mtu aliyejitambulisha kama John Maina Ndegwa aliwaambia polisi hao kuwa yeye ni wakili wa Kangethe na akasema alitaka kumuona.

Kangethe aliondolewa kwenye seli yake na kisha yeye na Ndegwa wakaachwa kwenye ofisi, lakini muda mfupi baadaye, mtuhumiwa huyo alitoroka na kumuwacha wakili wake, ambaye amewekwa kizuizini.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live