Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtu mmoja aaga, wengine 9 walazwa hospitalini baada ya kubugia pombe haramu

08a93afe7efcd7ac Mtu mmoja aaga, wengine 9 walazwa hospitalini baada ya kubugia pombe haramu

Mon, 12 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Watu 9 wamelazwa katika hospitali ya Nyahururu baada ya kudaiwa kunywa pombe yenye sumu siku ya Jumapili, Julai 11Hata hivyo, mtu mmoja aliaga dunia baada ya kunywa pombe hiyo Afisa mkuu wa afya eneo hilo aliwaonywa wakazi dhidi ya kunywa vileo kutoka kwenye maduka ambayo hayana leseni akishinikiza watakuwa wanahatarisha maisha yaoMtu mmoja ameaga dunia na wengine 9 kulazwa hospitalini baada ya kunywa pombe haramu eneo la Nyahururu siku ya Jumapili, Julai 11.

Kulingana na Daktari Felix Masongo wa hospitali ya Nyahururu ambaye aliwahudumia waathiriwa, alisema walifikishwa hospitali humo wakitapika na kulalamikia maumivu ya tumbo.

Masongo alisema wagonjwa hao walichukuliwa kutoka maeneo tofauti wengi wao wakiwa hali mbaya. Hata hivyo, watatu walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani.

Japo haijabainika ni pombe ipi waliokunywa, lakini wakazi wanaamini ilikuwa na sumu, Dkt Masongo amesema amechukua sampo kutoka kwa waathiriwa ambazo zinafanyiwa vipimo kubaini chanzo cha kifo cha mmoja wao.



Read also

Earth is Hard: Wanamtandao Wamcheka Ken Wakuraya Baada ya Kushindwa Kumpata Muthoni

Afisa mkuu wa afya kaunti ya Laikipia Donald Mugoi amewataka wale ambao pia huenda walikunywa pombe hiyo wafike hospitalini watibiwe kabla ya maafa zaidi kutokea.

" Tuna waomba wale wote ambao walikunywa pombe karibu na soko ya Nyahururu, waende hospitalini watibiwe. Nawahakikishia kwamba hawatakamatwa lakini ni kwa usalama wa afya yao," Alisema Mugo.

Mugoi pia aliwaonywa wakazi dhidi ya kunywa vileo kutoka kwenye maduka ambayo hayana leseni akishinikiza watakuwa wanahatarisha maisha yao na kuifanya kuwa ngumu kuwakamata wanaofanya biashara haramu.

Mmoja wa wakazi aliambia vyombo vya habari kwamba mmoja wa wafanyabiashara wa pombe hiyo anajulikana lakini serikali ya kaunti hajachukua hatua ya kumkamata.

Aidha, wakazi sasa wametaka serikali kufanya msaka na kuwakamatwa wote wanaoendesha biashara ya aina hiyo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.



Read also

Mombasa: Mganga Akamatwa na Kupokonywa KSh18M, Magari ya Kifahari ya KSh 30M
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke