Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtoto wa rais wa zamani wa Msumbiji ahukumiwa miaka 12 jela kwa ufisadi

Mtoto Wa Rais Wa Zamani Wa Msumbiji Mtoto wa rais wa zamani wa Msumbiji ahukumiwa miaka 12 jela kwa ufisadi

Thu, 8 Dec 2022 Chanzo: Voa

Mahakama moja nchini Msumbiji leo Jumatano imewahukumu wakuu wawili wa zamani wa ujasusi na mtoto wa rais wa zamani kifungo cha miaka 12 jela kila mmoja kwa kuhusika kwao katika kashfa ya ufisadi ambapo serikali ilificha madeni makubwa, na kusababisha mzozo wa kifedha nchini humo.

Miongoni mwa washtakiwa 19 walioshtumiwa katika kashfa kubwa nchini humo ni mtoto wa rais wa zamani Armando Guebuza, Ndambi Guebuza, mkuu wa zamani wa idara ya usalama na ujasusi, Gregorio Leao, na mkuu wa zamani wa idara ya ujasusi kuhusu masuala ya uchumi ambaye aliongoza kampuni tatu za serikali zilizokopa mabilioni ya pesa katika njia isiyo halali, Antonio do Rosario.

Washtakiwa wanane waliachiwa huru huku waliobaki wakipewa kifungo cha kati ya miaka 10 na 12.

Kashfa hiyo iliibuka baada ya kampuni za serikali katika nchi hiyo kukopa kinyume cha sheria dola bilioni 2 mwaka wa 2013 na 2014 kutoka benki za kimataifa ili kununua meli ya uvuvi na meli za usalama.

Chanzo: Voa