Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtoto wa Raila asema atafanya harusi yake Ikulu

3309044e198741ac Mtoto wa Raila asema atafanya harusi yake Ikulu

Wed, 13 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Bintiye kinara wa chama cha ODM Raila Odinga Winnie Odinga ametangaza kwamba ataolewa mwaka wa 2022 baada ya babake kushinda uchaguzi wa urais.

Bintiye Raila huenda akafunga pingu za maisha mwaka ujao iwapo babake atakuwa Rais baada ya uchaguzi mkuu. Winnie alisema ataolewa pindi tu babake atakapoingia ikulu 2022. Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 31 aliyasema haya akiwa kwenye mkutano na vijana kutoka Mlima Kenya siku ya Jumanne, Oktoba 12Raila anaazimia kuwa Rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya na amekuwa akizuru sehemu mbali mbali za nchi kujipigia debe.

Akimjibu seneta mteule Ngugi ambaye alidai kwamba anamtafuta mke wa kuoa, Winnie alisema kwamba atafunga pingu za maisha hivi karibuni lakini kwa masharti kadhaa.

Akizungumza Jumanne, Oktoba 12 kwenye mkutano na vijana kutoka Mlima Kenya uliohudhuriwa na Raila, Winnie aliwaalika Wakenya kwenye harusi yake ambayo alisema itafanyika katika ikulu 2022.

" Waambie kwamba nilisema Winnie Odinga ataolewa mwaka wa 2022 akiwa katika ikulu ya Nairobi, nyote mmekaribishwa, kwa hivyo iwapo mnataka haya yote kutendeka basi nendeni mkajisajili kama wapiga kura," Winnie alisema.

Kwa mara kadhaa, Winnie amekuwa akiwapuuza baadhi ya wanaume ambao wamekuwa wakimuomba posa akidai kwamba wakati ufaao haujafika yeye kuolewa.

Raila anaazimia kuwa Rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya na amekuwa akizuru sehemu mbali mbali za nchi kujipigia debe.

Tayari magavana zaidi ya watano kutoka eneo la Mlima Kenya linaloaminika kuwa ngome ya Raila wamemuidhinisha kuwania kiti hicho.

Baadhi ya magavana hao ambao kwa sasa wanaimba lugha moja na Raila ni Nderitu Muriithi (Laikipia), Lee Kinyanjui (Nakuru), James Nyoro (Kiambu), na Francis Kimemia (Nyandarua).

Kumekuwa na tetesi kwamba huenda gavana Lee Kinyanjui akawa mgombea wa urais wa Raila Odinga ingawa chama cha ODM hakijatoa taarifa kamili.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke