Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtoto wa Museveni ameonya jeshi la Uganda dhidi ya kushambulia M23

Mtoto Wa Museveni Ameonya Jeshi La Uganda Dhidi Ya Kushambulia M23 Mtoto wa Museveni ameonya jeshi la Uganda dhidi ya kushambulia M23

Tue, 22 Nov 2022 Chanzo: Bbc

Mtoto wa rais wa Uganda ameonya jeshi la nchi hiyo kuacha kudhihaki kundi la waasi la M23 akiwaita waasi hao kuwa ndugu zake.

Muhoozi Kainerugaba, ambaye ni Jenerali katika jeshi la Uganda UPDF, ameandika ujumbe wa twiter wakati Uganda inatayarisha wanajeshi 1000 kuingia Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo kupambana na kundi la waasi la M23.

Alikuwa kamanda wa kikosi cha jeshi la ardhini kinachoenda kupigana DRC, kabla ya kupandishwa cheo na kuwa Jeenerali na kuondolewa kuwa kamanda wa kikosi hicho.

Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ambaye ni mtoto wa rais Yoweri Museveni, amekuwa akiandika ujumbe wa twiter kuunga mkono waasi wa M23.

Ujumbe wake wa kuonya jeshi la UPDF, ambalo analitumikia, unajiri siku chache baada ya naibu wa mkuu wa jeshi la Uganda Luteni Jenerali Peter Elwelu, kusema kwamba jeshi la Jumuiya ya Afrika mashariki lina uwezo wa kusambaratisha waasi wa M23 katika muda was aa 24.

“Nilisikia baadhi ya watu wakisema kwamba wanaweza kuwashinda nguvu M23 katika muda wa siku moja? Sawa, hivyo ndivyo Obote alikuwa akisema kuhusu NRA wakiwa Luweero,” ameandika Muhoozi.

Milton Obote, alikuwa rais wa Uganda wakati Yoweri Museveni na waasi wake wa National resistance Army NRA walikuwa Luweero, wakipigana kuelekea Kampala. Museveni na waasi wa NRA walipigana na kupindua serikali. Amekuwa madarakani tangu mwaka 1986.

Muhoozi ameendelea kusema kwamba waasi wa M23 wanastahili “kubembelezwa ili kuacha kupigana kwa ajili ya amani na kwamba watakubali hatua hiyo kwa sababu wanapenda DRC iwe na amani.”

Mapema mwezi uliopita, Muhoozi Kainerugaba aliandika ujumbe kuunga mkono waasi wa M23, akisema kwamba “uasi wao ni wa haki.”

“Ni hatari sana kwa mtu yeyote kupigana na hao ndugu wetu. Sio magaidi! Wanapigania haki za Watutsi wanaoishi DRC,” aliandika Muhoozi kwenye twiter.

Chanzo: Bbc