Hatimaye mtoto wa aliyekuwa Rais wa Libya, Muammar Gaddafi, Saif al-Islam Gaddafi’s ameshinda hukumu ya rufaa aliyokata katika Mahakama ya Sebha huko Libya kuhusu kuondolewa kwenye kinyang’anyiro cha kiti cha Urais wa nchi baada ya kutuhumiwa kuwa na rekodi za uhalifu wa kivita.
Hatimaye mtoto wa aliyekuwa Rais wa Libya, Muammar Gaddafi, Saif al-Islam Gaddafi’s ameshinda hukumu ya rufaa aliyokata katika Mahakama ya Sebha huko Libya kuhusu kuondolewa kwenye kinyang’anyiro cha kiti cha Urais wa nchi baada ya kutuhumiwa kuwa na rekodi za uhalifu wa kivita. Mwanasheria wa Saif Gaddafi, Khaled al-Zaydi amesema hukumu hiyo imerejesha matumaini kwa mteja wake kushiriki uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Desemba 24 akiwa mgombea wa kiti cha Urais.