Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtangazaji Bonnie Musambi Kuondoka KBC baada ya Kuhudumu Miaka 14

692acc5ae1c3cec9 Mtangazaji Bonnie Musambi Kuondoka KBC baada ya Kuhudumu Miaka 14

Tue, 6 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Bonnie anaondoka KBC kuanzisha kituo chake cha radio ya lugha ya Kamba, Sang'u FM

- Mwandani wa mtangazaji huyo alidokezea kwamba ana mpango wa kutengana na shirika hilo la serikali

- Musambi atatumia kituo chake kuwakuza wanahabari chipukizi

Mtangazaji tajika Bonnie Musambi anatazamiwa kujiuzulu kutoka kwa Shirika la Habari la (KBC) baada ya kuhudumu kwa miaka 14.

Katika KBC, mtangazaji huyo huendesha shoo ya asubuhi kwa jina Zinga la Asubuhi pamoja na Cynthia Anyango na pia husoma habari kwenye KBC Channel 1.

Duru ilidokezea TUKO.co.ke kuwa Bonnie anaondoka KBC kuanzisha kituo chake cha radio ya lugha ya Kamba, Sang'u FM.

"Bonnie ataondoka KBC baadaye mwaka huu kufungua kituo chake cha Sang'u FM. Mipango iko tayari kile kimesalia ni kituo cha Musambi kupepea hewani," ilidokezea duru hiyo.

Mwandani wa mtangazaji huyo alidokezea kwamba amekuwa na mpango wa kutengana na shirika hilo la serikali.

Musambi atatumia kituo chake kuwakuza wanahabari chipukizi.

Katika njia ya kuwashikilia mashabiki wake, ataendesha kipindi cha Kiswahili, ambapo ataendelea kuonyesha talanta yake ya kuwapatanisha watu kama afanyavyo kwenye Radio Taifa katika kitengo cha Ujumbe Maalum.

TUKO.co.ke imetambua kuwa tayari kituo hicho kimewanasa watangazaji tajika wa lugha ya Kikamba na kabila zingine

Kwa sasa inasimamiwa na mke wa mtangazaji huyo Betty Musambi, ambaye pia ni mwanahabari.

Kituo hicho ambacho kitakuwa kinapeperisha matangazo yake kutoka Nairobi, pia kitakuwepo mtandaoni.

Awali Musambi alikuwa ametangza kuwa atawania kiti cha ubunge cha Kituo Kaskazini mwaka 2022.

Katika taarifa tofauti, mtangazaji huyo alimsifu mke wake kwa kuhakikisha kuwa watoto wake wanalelewa vyema shuleni na nyumbani.

Musambi alikiri kwamba kazi yake humfanya kuondoka nyumbani mapema na kumshukuru mke wake kwa kuhakikisha wanao wanakwenda shuleni wakiwa na furaha.

Musambi kupitia Instagram alimsherehekea mkewe kwa juhudi zake za kutekeleza wajibu wake kama mama.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke