Polisi nchini Afrika Kusini wanachunguza mauaji ya mtalii mmoja raia wa Ujerumani ambaye amepoteza maisha katika jaribio la kuteka gari lililotokea mashariki mwa jimbo la Mpumalanga.
Raia huyo wa Ujerumani alikua sehemu ya kundi la watalii wanne ambao pia ni raia wa Ujerumani waliofika nchini humo kutalii.
Tukio hilo limetokea jumatatu ya jana jioni wakati wajerumani hao walipokua wanaelekea kwenye vyumba vya mapumziko wakitokea hifadhi ya Taifa ya nchi hiyo ya Kruger .
Kundi la wahalifu linasemekana kuwaamrisha watalii waliokuwemo kwenye gari hilo kufungua milango ya gari lao , lakini dereva alifunga milango yote ambapo mmoja wa wahalifu alifyatua risasi kupitia dirishani na kumuua mtalii huyo papo hapo.
Baada ya tukio hilo kundi hilo la wahalifu lilitokomea bila kuchukua chochote , ambapo mkuu wapolisi wa eneo hilo Bw.Semakaleng Daphney Manamela ameliita tukio hilo kuwa ni la kikatili sana.